Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 8 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 87 2019-02-06

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakarabati mifereji ya maji ya mvua na kuta za mito inayoingiza maji ya bahari katika Mji wa Mikindani ili kuirejesha katika hali yake ya awali?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hawa Abdulrahman Ghasia, Mbunge wa Mtwara Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 kifungu cha 129(1) kinaeleza wajibu wa kila mamlaka ya Serikali za Mitaa kwenye eneo lake itajenga au kuandaa mifereji ya maji ya mvua.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kumekuwepo na changamoto ya kujaa kwa maji katika maeneo mengi nchini yanayopakana na bahari kunakosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi na hivyo kufanya baadhi ya mifereji kushindwa kumudu athari zake. Kufuatia hali hii, Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira imeanza kuchukua hatua zinazolenga kuzuia na kupunguza madhara yaliyojitokeza katika maeneo yaliyoathirika nchini ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini ya jumla ya maeneo haya ikiwemo Mikindani ili kuwezesha kuandaa Mpango wa Taifa wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali ipo katika hatua za kuandaa Mpango Endelevu wa Kitaifa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi (National Adaptation Plans) wenye malengo ya muda wa kati na muda mrefu ili kuboresha usimamizi wa mabadiliko nchini kwa kushirikiana na halmashauri zote.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kujenga uwezo wa kuhimili athari za mabadiliko ya tabia nchi, tunashauri halmashauri za maeneo husika kuingiza gharama za ukarabati wa mifereji kwenye bajeti zao ili kupunguza athari zilizozidi kuongezeka kwa kuiga mfano wa Jiji la Dar es Salaam.