Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Mji Mdogo wa Bagamoyo ulianzishwa tarehe 15/6/ 2005. Mwaka 2013/2014 Mamlaka hiyo iliiomba Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupewa hadhi ya Halmashauri ya Mji baada ya kujiridhisha kuwa na sifa stahili. Je, ni lini Serikali itaipa Bagamoyo hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na nitahamasisha wadau kuvuta subira. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunaendelea na mchakato wa kupata Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo, je, ni lini Serikali itawaagiza Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kuwalipa Wenyeviti wa Vitongoji malimbikizo yao ya posho ambayo hayajalipwa kwa mda mrefu sasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa vile Bagamoyo siyo Halmashauri ya Mji kwa hiyo hatuna fursa ya mafungu makubwa ya ujenzi wa miundombinu ya barabara. Sasa naomba kujua ni nini kauli ya Waziri kuhusu kutusaidia Bagamoyo mafungu ambayo yatatuwezesha kujenga miundombinu ya barabara na mifereji ambayo iko katika hali mbaya sana katika Mji wa Bagamoyo na Vijiji vya Bagamoyo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze na kumshukuru kwa kukubaliana na majibu kwenye swali la msingi na hili la kuwaomba wananchi wawe na subira wakati mchakato unaendelea, namshukuru sana kwa hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza amesema kwamba Wenyeviti wa Vitongoji hawajalipwa kwa muda mrefu na mimi napenda kumhimiza Mkurugenzi wa Halmashauri wa Wilaya ya Bagamoyo kutekeleza maagizo ya Serikali ambayo yanamtaka arejeshe asilimia 20 ya mapato yanayokusanywa kutoka kwenye kata husika ili yatumike, pamoja na kazi zingine, kulipa posho za Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji kwenye maeneo yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili amesema Mji wa Bagamoyo kweli una mahitaji ya miundombinu kama barabara na mifereji na amesema kwa usahihi kabisa kwamba itakapokuwa ni Halmashauri ya Mji ambayo inatakiwa iwe na sifa fulani kwa upande wa miundombinu sasa tuanze kupeleka mafungu kwa ajili ya kuanza ujenzi wa miundombinu hiyo. Mimi namuomba sana Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane hata baada ya Kikao hiki cha Bunge ili tuone ni namna gani mwakani tunaingiza kwenye bajeti ya TARURA huu ujenzi wa miundombinu ambao anaipendekeza.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Mji Mdogo wa Bagamoyo ulianzishwa tarehe 15/6/ 2005. Mwaka 2013/2014 Mamlaka hiyo iliiomba Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupewa hadhi ya Halmashauri ya Mji baada ya kujiridhisha kuwa na sifa stahili. Je, ni lini Serikali itaipa Bagamoyo hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji?

Supplementary Question 2

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwa Bagamoyo, Mji Mdogo wa Mbalizi ulianza mchakato wa kuomba iwe ni Halmashauri ya Mji kwa muda mrefu sana. Je, ni lini Serikali itaipa Mbalizi kuwa na hadhi ya Halmashauri ya Mji? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama wanavyofahamu Wabunge wengi sana humu, kuna mapendekezo mbalimbali ya maeneo mbalimbali kuanzisha mamlaka mpya lakini najua kwamba Mbalizi ni miongoni mwa maeneo ambayo yalikuwa katika mchakato wa kupandishwa hadhi, lakini nimuombe Mheshimiwa Mbunge kwamba tuvute subira kwa sababu mpango wa Serikali wa sasa hivi wa maelekezo ni kutoanzisha mamlaka mpya lakini kwa vile jambo hili liko katika subira tuvute subira pale hali itakapokuwa sasa imekaa vizuri Mji wa Mbalizi ni miongoni mwa miji ambayo itapewa kipaumbele cha kwanza katika upandishaji wa hadhi. (Makofi)