Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 session 13 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 17 2018-11-07

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-
Mji Mdogo wa Bagamoyo ulianzishwa tarehe 15/6/ 2005. Mwaka 2013/2014 Mamlaka hiyo iliiomba Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupewa hadhi ya Halmashauri ya Mji baada ya kujiridhisha kuwa na sifa stahili.
Je, ni lini Serikali itaipa Bagamoyo hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa sheria za Serikali za Mitaa Sura 287 (Mamlaka za Wilaya) na Sura 288 (Mamlaka za Miji), pamoja na mwongozo wa Serikali kuhusu uanzishwaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wa Mwaka 2014, mapendekezo ya kupandisha hadhi Mamlaka ya Mji Mdogo kuwa Halmashauri ya Mji yanapaswa kujadiliwa kwanza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kabla ya kuwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa uamuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa maombi hayo yalijadiliwa katika Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo tarehe 28, Septemba, 2018 (mwaka huu), na Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) tarehe 06, Oktoba, 2018 na kwa kuwa hayajajadiliwa kwenye Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) ambao wamepanga kikao hivi karibuni, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inamuomba Mheshimiwa Mbunge awaarifu wadau wa Mji wa Bagamoyo wawe na subira hadi taratibu hizo zitakapokamilika na uamuzi kufikiwa.