Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. AGNESS M. MARWA) aliuliza:- Wananchi wengi walibomolewa nyumba zao na Mgodi wa ACACIA uliopo Nyamongo, Mkoani Tarime na wengine hawajalipwa fidia ya maeneo yao mpaka sasa. Aidha, Mgodi huo pia umeanza kuchimba chini ya ardhi ya maeneo ya watu (underground mining):- Je, ni lini Mgodi wa ACACIA uliopo Nyamongo utalipa fidia kwa wananchi hao?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeze tu Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali kwa jinsi wanavyoshughulikia suala hili katika Mgodi ule wa ACACIA Nyamongo kule. Nina maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tatizo la fidia katika eneo la Nyamongo limekuwa la muda mrefu; na ni miaka mingi kila siku watu wanadai na wengine wanadai malipo hewa na wengine malipo halali: Ni lini sasa Serikali itamaliza hili tatizo kwa muda muafaka ili kutufa kabisa tatizo la kudai madai ya Nyamongo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, matatizo yanayotokea Nyamongo, yanafanana sana na matatizo yanayotokea katika kijiji changu cha Nyabuzume Jimbo la Bunda Kata ya Nyamang’uta; na kwa bahati nzuri Mheshimiwa Naibu Waziri wewe ulifika kenye kile kijiji, kuna wachimbaji wako pale, wanapiga yowe za muda mrefu, wanasumbua wananchi na hawawezi kushirikiana nao katika kupeana zile kazi za kijiji; nawe uliahidi kumaliza hilo tatizo. Ni lini tatizo la Nyabuzume wale wachimbaji wasio halali au walio halali ambao hawatekelezi suala la kuondoa matatizo ya wanakijiji katika kijiji kile?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza Mheshimiwa Getere, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa madai ya Nyamongo kule North Mara katika ile kampuni ya Acacia yamechukua muda mrefu. Yamechukua muda mrefu kwa sababu mbili. Sababu ya kwanza ni kampuni yenyewe ya Acacia ilichelewa kulipa malipo kwa muda uliostahili. Sababu ya pili ni kwa wananchi wenyewe ambao baada ya evaluation ya kwanza ku-expire, evaluation ya pili kuna watu walifanya speculation, yaani walifanya kutegesha, kwa maana waliongeza majengo, wakaongeza mazao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli limetupa shida sana suala hili kwa sababu evaluation ya mwanzo ilikuwa inaonekana ni ndogo, kuja kufanya evaluation ya pili imeonekana ni kubwa sana. Mfano kuna sehemu ya Nyabichele. Wao walithaminishiwa kwenye mazao yao; gharama ilikuwa ni shilingi bilioni 1.6, lakini baada ya evaluation ya pili kuja kufanyika, gharama yake ikaonekana ni shilingi bilioni 12. Hili limefanya kampuni kusita kuweza kulipa fedha hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya msingi nilisema kwamba hili suala lipo kwa Chief Valuer na leo nimeongea na Chief Valuer amefanya evaluation na ameandika barua kwa North Mara kwa maana ya Kampuni ya Acacia, ile evaluation ambayo wameandikiwa na Chief Valuer wailipe immediately. Wailipe mara moja, wasipoteze
muda ili kuondoa manung’uniko. Vilevile kupitia Serikali ya Mkoa wa Mara, tumeelewana na Kampuni ya Acacia kwa maana ya North Mara, walipe fidia kwa wale wananchi wanaodai wanaona kabisa kwamba wananchi hawa wana madai yao ya haki, hawana dispute yoyote, hawana mgogoro wowote, hao walipwe mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuna wananchi wengine ambao ni 138 toka mwaka 2016 kuna cheque ya thamani ya shilingi bilioni 3.2 wamegoma kwenda kuchukua kwa sababu wanalishana maneno, wanasema kwamba wanacholipwa ni kidogo. Nawaasa na ninawaomba, wananchi ambao cheque zao ziko tayari, waende wakachukue cheque zao mara moja ndani ya wiki hii. Wasipochukua ina maana sasa Serikali ya Mkoa itachukua hatua nyingine na itakuwa vinginevyo. Kwa hiyo, itazidi kuwacheleweshea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, nawaomba wananchi wa Mkoa wa Mara na maeneo ya North Mara tusilishane maneno. Watu ambao wana haki, wanatakiwa kulipwa na cheque zao ziko kihalali, waende wakachukue cheque zao mara moja. Kampuni ya North Mara, ndani ya wiki hii tumeshawaambia, yale maeneo ambayo hakuna dispute, walipe mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuhusiana na suala la Bunda kule ambako Mheshimiwa Mbunge amelielezea, kwa wale watu wanaomiliki PLs na hawazitumii, nimezungumza hapa hata jana, kwamba kwa wamiliki wa PLs wasiozitumia, hawafanyi tafiti, sisi tunapitia PL moja baada ya nyingine. Tunakwenda kufuta hizo PL na tunakwenda kuwapa wachimbaji wadogo wachimbe ili waweze kujipatia kipato na Serikali iweze kupata mapato kupitia uchimbaji mdogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.