Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:- Barabara ya Surungaji inayoanzia Chikuyu - Chibumagwa - Majiri – Ikasi (Kilomita 76.2) ni barabara muhimu sana inayohudumia wakazi wa bonde la ufa katika Jimbo la Manyoni Mashariki kwa kusafirisha chumvi, samaki, ufuta na alizeti:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii pamoja na daraja katika Mto Nkonjigwe.

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Spika,ahsante kwa kunipa muda niweze kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza niipongeze sana Serikali na majibu imejibu vizuri, imepeleka faraja kwa wananchi wa Jimbo la Manyoni hasa Manyoni Mashariki, niombe kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara hii tunayoizungumzia ya Chikuyu Majiri-Ikasi, kipande kile cha mwisho kabisa cha kilometa 40kwa maana ya Majiri kwenda Ikasi, ni miaka zaidi ya 40 hakijapata fedha ya matengenezo ya mara kwa mara.

Naomba tu kuhakikishiwa na kuwahakikishia wananchi wangu wa Manyoni ni lini au ni bajeti ya mwaka huu watatoa fedha ya kutengeneza barabara hii maana ni miaka zaidi ya 40? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtuka Motokari kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika swali lake la nyongeza anasema miaka zaidi ya 40 barabara hii haijatengewa fedha yoyote, wakati mwingine mipango ya Mwenyezi Mungu inakuwepo ili mtu fulani aweke alama, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mtuka laiti barabara hiyo ingekuwa imetengenezwa isingekuwa kwake yeye rahisi kuacha alama, naomba nimhakikishie ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii inatengenezwa na hasa baada ya kujua gharama ya daraja ambalo ndiyo kubwa zaidi na yeye atakuwa ameacha alama muhimu sana kwa wananchi ambao miaka zaidi ya 40 ilikuwa haipitiki.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:- Barabara ya Surungaji inayoanzia Chikuyu - Chibumagwa - Majiri – Ikasi (Kilomita 76.2) ni barabara muhimu sana inayohudumia wakazi wa bonde la ufa katika Jimbo la Manyoni Mashariki kwa kusafirisha chumvi, samaki, ufuta na alizeti:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii pamoja na daraja katika Mto Nkonjigwe.

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Spika,nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya kutoka Singida – Kinyeto - Mahojoa - Sagara yenye urefu wa kilomita 42 ambao tuliiombea kwa Mheshimiwa Rais kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kweli kwa sasa imeharibika kwa kiwango kikubwa sana. Je, Serikali ipo tayari sasa kutenga fedha za ziada za dharura katika kuhakikisha kwamba madaraja yaliyovunjika katika msimu huuna barabara yanarekebishwa?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Monko anakiri kwamba barabara hiyo ilikuwa imejengwa kwa kiwango cha lami na mvua imenyesha madaraja yameanza kubomoka. Tukubaliane kwamba kila neema wakati mwingine inakuja na adha yake, kama ambavyo ilikuwa nia ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii inapitika, ni vizuri tukaenda tukajua uharibifu uliotokea na gharama zinazohitajika ili kuirudisha barabara katika hali yake ya kuweza kupitika kama tunavyotarajia kwa wananchi wetu.