Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 27 2019-01-31

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:-

Barabara ya Surungaji inayoanzia Chikuyu - Chibumagwa - Majiri – Ikasi (Kilomita 76.2) ni barabara muhimu sana inayohudumia wakazi wa bonde la ufa katika Jimbo la Manyoni Mashariki kwa kusafirisha chumvi, samaki, ufuta na alizeti:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara hii pamoja na daraja katika Mto Nkonjigwe.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Edward Mtuka, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Chikuyu- Chibumagwa –Majiri-Ikasi yenye urefu wa Kilomita 76.2 inahudumiwa na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni. Katika kilomita 76.2 ni kilomita 32 tu zinazopitika majira yote ya mwaka (kilomita 14.8 ni za changarawe na kilomita 18.8 ni za udongo), kilomita 4.2 ambazo ni kutoka majirimpaka Ikasi hupitika wakati wa kiangazi pekee.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Chibumagwa-Majiri- Ikasi ilitengewa kiasi cha Sh.29,500,000.00 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ambapo jumla ya kilomita tisa zilifanyiwa matengeneza (sehemu korofi kilomita saba na ya kawaida kilomita mbili) kuanzia Chikuyu-Chibumagwa na kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kiasi cha Sh.11,600,000.00 kimetumika kujenga makalavati (line culvert)mbili katika eneo la Mpandagani kwenye barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2019/20 TARURA inatarajia kufanya usanifu wa Daraja la Mto Nkonjigwe lenye urefu wa mita 35 na kina cha mita sita lililopo barabara ya Chikuyu-Chibumagwa-Majiri-Ikasi. Fedha za ujenzi zitatengwa kwenye bajeti baada ya usanifu ili tuweze kujuwa gharama halisi.