Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE (K.n.y MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA) aliuliza:- Kwa kuwa Serikali ina mkakati madhubuti wa kupunguza vifo vya akina mama na watoto:- (a) Je, ni lini Zahanati ya Kiboga katika Kata ya Msongola itafunguliwa ili wananchi wapate huduma ya afya? (b) Kwa kuwa wananchi wa Mtaa wa Mbondole katika Kata ya Msongola walitoa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, je, ni lini zahanati hiyo itakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na majibu mazuri ya Serikali, naomba nimuulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, tatizo la zahanati katika nchi yetu limekuwa likipungua siku hadi siku lakini kwa baadhi ya maeneo, maeneo mengi wananchi wameweza kuweka nguvu kazi zao kuhakikisha kwamba zahanati zinapatikana ili kupunguza vifo vya akina mama na watoto. Je, lini Serikali itamaliza yale maboma yote kuhakikisha kwamba tatizo hili linaisha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, swali hili linarandana sana na kituo cha afya kilichopo kule Lindi katika Kata ya Mnazi Mmoja. Je, ni lini watawahakikishia wananchi wa Lindi wanamaliza lile jengo pamoja na kwamba wameshawapa kiasi fulani cha fedha? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la kumalizia maboma ambayo wananchi wameingiza nguvu zao, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Salma, naye ni shuhuda, jinsi ambavyo Serikali inaelekeza nguvu zake kuhakikisha kwamba maboma yote tunayamalizia hatua kwa hatua. Ndiyo maana tumeanza na ujenzi na ukamilishaji wa vituo vya afya 208 na juzi vimeongezeka viwili, tumekuwa na 210. Naomba nimhakikishie kwamba jitihada ambazo zimefanywa na wananchi Serikali itahakikisha kwamba tunamalizia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili linalohusiana na Kituo cha Afya cha Mnazi Mmoja, naomba nimpongeze Mheshimiwa Salma kwa jitihada zake za kuwapigania wananchi wa Mkoa wa Lindi. Nilipata fursa ya kwenda kutizama kazi ya ujenzi wa Kituo cha Afya Lindi, kazi niliyoiacha ilikuwa inaenda vizuri. Naamini katika muda ambao tumekubaliana kwamba vituo vya afya hivi vijengwe kwa kuzingatia miezi mitatu na wananchi wa Lindi kwa maana ya Kituo cha Afya Mnazi Mmoja kwa jitihada nilizoziona na nguvu kazi na ari yao ya kujitoa, naamini ndani ya muda huo kituo cha afya kitaweza kukamilika. (Makofi)

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE (K.n.y MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA) aliuliza:- Kwa kuwa Serikali ina mkakati madhubuti wa kupunguza vifo vya akina mama na watoto:- (a) Je, ni lini Zahanati ya Kiboga katika Kata ya Msongola itafunguliwa ili wananchi wapate huduma ya afya? (b) Kwa kuwa wananchi wa Mtaa wa Mbondole katika Kata ya Msongola walitoa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, je, ni lini zahanati hiyo itakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Katika mkakati wa kupunguza vifo vya mama na mtoto Jimboni Igalula tumeanzisha ujenzi wa vituo vya afya vitano kwa nguvu za wanachi na Mbunge ambapo tumefikia katika hatua ya boma. Je, Serikali ina mpango gani kusaidia nguvu hizi za wananchi ukizingatia hatuna kituo hata kimoja cha afya katika Jimbo la Igalula? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri sana, yale ya wali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali hili la Mheshimiwa Ntimizi, kwanza naomba nimpongeze Mbunge huyu, katika kazi ambayo ameifanya ni kuhamasisha wananchi wake kujenga vituo vya afya vipya lakini bado havijajengwa. Nikiri wazi kwamba amefika ofisini kwangu na kuweza kuweka kipaumbele katika suala zima la Jimbo lake. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama tulivyoongea ofisini kwetu jinsi gani tutafanya ofisi yetu isaidie katika suala zima maeneo yale tupate vituo vya afya hasa tukianza na vituo vya afya viwili, jambo hili ni commitment ya Serikali, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo ili wananchi wa eneo lile la Jimbo la Igalula waweze kupata huduma ya afya.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE (K.n.y MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA) aliuliza:- Kwa kuwa Serikali ina mkakati madhubuti wa kupunguza vifo vya akina mama na watoto:- (a) Je, ni lini Zahanati ya Kiboga katika Kata ya Msongola itafunguliwa ili wananchi wapate huduma ya afya? (b) Kwa kuwa wananchi wa Mtaa wa Mbondole katika Kata ya Msongola walitoa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, je, ni lini zahanati hiyo itakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupunguza vifo vya akina mama wajawazito ni pamoja na uwepo wa vifaa vya kujifungulia katika hospitali zetu lakini mpaka hivi tunavyozungumza, ziko hospitali, zahanati na vituo vya afya akina mama wanatakiwa waende na mabeseni na mipira kwa ajili ya kujifungua. Ni lini tatizo hili litarekebishwa na Serikali yetu? Ahsante. (Makofi

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Sikudhani Chikambo, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna changamoto ya vifaa mbalimbali lakini lazima tumshukuru Mheshimiwa Rais, tukumbuke hapa katikati aliweza kutoa vifaa kwa karibu Halmashauri zote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na uboreshaji wa vituo hivi vya afya 208 tunavyovijenga ambavyo jumla yake pamoja na vifaa itagharimu karibu shilingi bilioni 156, naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge wote siyo muda mrefu sana vituo hivi vinavyokamilika, vifaa hivi tutavisambaza maeneo mbalimbali. Ni imani yangu kubwa kwamba tutapunguza kero kubwa sana katika suala zima la vifaa vya kujifungulia katika vituo vyetu vya afya na zahanati zetu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.