Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 343 2018-05-31

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE (K.n.y MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA) aliuliza:-
Kwa kuwa Serikali ina mkakati madhubuti wa kupunguza vifo vya akina mama na watoto:-
(a) Je, ni lini Zahanati ya Kiboga katika Kata ya Msongola itafunguliwa ili wananchi wapate huduma ya afya?
(b) Kwa kuwa wananchi wa Mtaa wa Mbondole katika Kata ya Msongola walitoa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa zahanati, je, ni lini zahanati hiyo itakamilika?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiboga na Luhanga ni mitaa miwili inayopakana ambayo hapo awali ilikuwa miongoni mwa vitongoji katika Kijiji cha Mvuti, Kata ya Msongola. Wananchi wa Mtaa wa Luhanga kwa nguvu zao wenyewe walianza ujenzi wa zahanati na Serikali ikawaunga mkono na sasa jengo la zahanati ya Luhanga lipo katika hatua za upakaji rangi, kuweka madirisha na milango. Mtaa wa Kiboga bado hauna zahanati hivyo halmashauri inatakiwa kutenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa zahanati. Hata hivyo, wakazi wa Kiboga wanapata huduma za afya katika Zahanati ya Mvuti ambayo ipo ndani ya kilometa tano ambayo ni matakwa ya utekelezaji wa Mpango Maalum wa Uimarishaji Afya ya Msingi 2009 - 2017.
b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Zahanati ya Mbondole imebaki kupigwa rangi na kuwekewa milango ili ikamilike na kuanza kutoa huduma. Halmashauri ya Wilaya ya Ilala imetenga shilingi milioni 70 katika mwaka wa fedha 2017/2018 ambayo inaweza kukamilisha ujenzi huo.