Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Kata ya Bukene Wilayani Nzega inaundwa kwa Kijiji kimoja tu chenye wakazi zaidi ya 7,600 jambo ambalo linakwamisha uharakishaji wa huduma za maendeleo kwa wananchi. Tulishafuata taratibu zote za kuomba Kijiji cha Bukene kigawanywe ili kupata Kijiji kingine kipya:- Je, Serikali haioni kuwa siyo sahihi kuwa na Kata inayoundwa na Kijiji kimoja?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana taarifa kwamba mchakato huu wa kuomba Mji wa Bukene upandishwe hadhi ulianza siku nyingi na mpaka Wizara ikatoa GN Namba 176 ya mwaka 1996 ambayo mpaka sasa haijafanyiwa mchakato wowote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwenye swali langu la msingi niliuliza, je, muundo wa kuwa na Kata moja inayoundwa na Kijiji kimoja tu ni sahihi? Kwa sabbau muundo huu unapelekea Mtendaji wa Kijiji kutokuwa na tofauti yoyote na Mtendaji wa Kata na Serikali ya Kijiji haina tofauti yoyote na WDC na ni sawa sawa na kuwa na Mkoa mmoja unaoundwa na Wilaya moja tu ambayo kutakuwa hakuna tofauti yoyote ya Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa, kwa sababu mkoa ni mmoja na Wilaya ni mmoja. Je, muundo huu ni sahihi kuwa na Kata moja ambayo inaundwa na Kijiji kimoja tu? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza ananiuliza kama najua kwamba kuna GN ambayo ilikuwa imetolewa na kwamba mpaka sasa hivi GN hiyo haijafanyiwa marekebisho yoyote, taarifa hiyo ninayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, anauliza uwezekano wa Kijiji hicho kimoja kikawa Kata, naomba nitoe ufafanuzi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Selemani Zedi anajua kwamba ilikuwa mchakato wa kupandisha Kijiji cha Bukene kuwa Halmashauri ya Mji Mdogo na Bukene kama ilivyo ina vitongoji vyake 11 na lengo lilikuwa hivyo Vitongoji vije vibadilike kuwa Mitaa ambayo ingeweza kutosha katika kubadilisha sasa kuwa na Mamlaka ya Mji Mdogo wa Bukene. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Selemani Zedi, taratibu hizo zingine ziendelee ili ukifika wakati ambapo Serikali itakuwa tayari kuongeza maeneo ya kiutawala na Bukene iwe na sifa ya kuweza kuongezeka.

Name

Justin Joseph Monko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Kata ya Bukene Wilayani Nzega inaundwa kwa Kijiji kimoja tu chenye wakazi zaidi ya 7,600 jambo ambalo linakwamisha uharakishaji wa huduma za maendeleo kwa wananchi. Tulishafuata taratibu zote za kuomba Kijiji cha Bukene kigawanywe ili kupata Kijiji kingine kipya:- Je, Serikali haioni kuwa siyo sahihi kuwa na Kata inayoundwa na Kijiji kimoja?

Supplementary Question 2

MHE. JUSTIN J. MONKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kijiji cha Ndwamughanga kilichopo katika Jimbo la Singida Kaskazini kina vitongoji ambavyo vipo Mukulu ambavyo viko kilomita 23 kutoka Makao Makuu ya Kijiji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukiomba Vitongoji hivi visajiliwe kama Kijiji kwa muda mrefu. Je, ni lini Vijiji hivi vya Mukulu vinaweza kupata usajili wa kuwa kijiji kinachojitegemea ukizingatia umbali ili wananchi waweze kupata huduma za Kiserikali?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema kuna Kitongoji ambacho kipo kilomita 20 kutoka katika Kijiji ambacho ndiyo kimezaa hicho Kitongoji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sifa za Kitongoji kutoka katika Kitongoji kuwa Kijiji sasa sina uhakika na sifa ya hicho Kitongoji ambacho kinalazimika kufuata huduma ya kilomita 20. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kuzingatia vigezo na sifa za kitongoji kubadilika kuwa kijiji pindi zitakapokuwa zimekamilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI haitasita kuhakikisha kwamba Kitongoji hicho kinakuwa Kijiji kama sifa stahiki zinakidhi.

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza:- Kata ya Bukene Wilayani Nzega inaundwa kwa Kijiji kimoja tu chenye wakazi zaidi ya 7,600 jambo ambalo linakwamisha uharakishaji wa huduma za maendeleo kwa wananchi. Tulishafuata taratibu zote za kuomba Kijiji cha Bukene kigawanywe ili kupata Kijiji kingine kipya:- Je, Serikali haioni kuwa siyo sahihi kuwa na Kata inayoundwa na Kijiji kimoja?

Supplementary Question 3

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Nachingwea ina jumla ya Kata 36 na tayari inakidhi vigezo vya kupata Majimbo mawili ya uchaguzi na taratibu zote tumeshazifuata. Ni lini Wizara ya TAMISEMI itakwenda kuligawanya Jimbo la Nachingwea ili liwe na Majimbo mawili ya uchaguzi? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata fursa ya kwenda Wilaya ya Nachingwea na Jimbo la Nachingwea, kwa hiyo najua ambacho Mheshimiwa Mbunge anaongelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, zipo taratibu ambazo zinatakiwa zifuatwe ili Jimbo ligawanywe na hii huwa inapelekwa kwenye Tume ya Uchaguzi ndiyo wenye mamlaka ya kugawanya Majimbo na siyo Ofisi ya Rais, TAMISEMI.