Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:- (a) Je, ni utaratibu upi uliotumika na Serikali kuzuia malipo ya 80% kwa mwezi kwa Majaji Wastaafu ambayo ni haki yao ya msingi na malipo ya mafao yao yanayotambulika kwa mujibu wa Sheria ya Majaji? (b) Je, ni utaratibu upi unaotumika sasa kuzuia malipo hayo kwa baadhi ya Majaji?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba Wilaya ya Rufiji ni Wilaya kongwe. Ni miongoni mwa Wilaya za awali, ina miaka zaidi ya 55 toka izaliwe lakini kutokana na mgawanyo wa Wilaya, Wilaya hii imebaki kuwa ni Wilaya pekee ambayo haina Mahakama ya Wilaya. Wananchi wangu wanalazimika kusafiri umbali wa zaidi ya kilometa 100 kufuata huduma za Mahakama ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itakuwa na mpango wa kujenga Mahakama ya Wilaya kuwasaidia wananchi wangu wa Jimbo la Rufiji?
Mheshimiwa Naibu Spika, tofauti ya mshahara kati ya Hakimu na Jaji ni kubwa sana na kazi wanazofanya Mahakimu takribani ni kubwa kuliko wanazofanya Majaji. Nataka nifahamu Serikali inajipanga vipi kuboresha maslahi ya Mahakimu katika suala zima la mishahara, msaada wa nyumba (house allowance) pamoja na non-practicing allowance kwa Mahakimu nchi nzima?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA SHERIA NA KATIBA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuchomekea maslahi ya Jimbo lake la Rufiji katika swali hili. Naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara inaelewa hali maalum ambayo Jimbo lake inayo hasa baada ya kumegwamegwa, tumepata hapo Kibiti na Mafia na tunaelewa kabisa kwamba miundombinu ya Mahakama katika Jimbo lake ni mbaya. Naomba nimhakikishie katika mpango wa Mahakama wa miaka mitano, suala la miundombinu ya Mahakama ya Rufiji tutalitilia maanani sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu tofauti ya mishahara ya Mahakimu na Majaji, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba tunaangalia pia mishahara ya maafisa ya Mahakama walioko chini. La msingi tu ni kwamba ili kukidhi matakwa ya Kimataifa na pia matakwa yetu ya kikatiba, ni lazima tufikie vigezo vya kuwalipa Majaji vizuri wasiwe na vishawishi vya kuweza kuchukua rushwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri katika hili kwa upande wa Majaji Tanzania tumefanikiwa sana. Kazi yetu kubwa ni kuangalia Mahakama za chini siyo tu Mahakama za Hakimu Mkazi, Mahakama ya Wilaya lakini mpaka Mahakama za Mwanzo kwani kwa upande wa Mahakama za juu tumejitahidi. Nafikiri sisi ni moja ya nchi chache duniani ambazo kwa kweli tumefikia viwango stahili katika kujali maslahi ya Mahakama zetu za juu.

Name

Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:- (a) Je, ni utaratibu upi uliotumika na Serikali kuzuia malipo ya 80% kwa mwezi kwa Majaji Wastaafu ambayo ni haki yao ya msingi na malipo ya mafao yao yanayotambulika kwa mujibu wa Sheria ya Majaji? (b) Je, ni utaratibu upi unaotumika sasa kuzuia malipo hayo kwa baadhi ya Majaji?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sengerema hali haiko tofauti sana na Rufiji. Mahakama za Mwanzo tisa zilifungwa kwa sababu mbalimbali zaidi ya mwaka mmoja na nusu sasa. Je, upo utaratibu sasa katika Wizara yako unaoweza kuziwezesha Mahakama hizi kufunguliwa ili haki iweze kupatikana kirahisi kwa wananchi?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nina bahati kwamba, mwezi uliopita nilitembelea Jimbo la Sengerema na Buchosa. Kwa kweli hali ya miundombinu ya Mahakama hata mimi mwenyewe nimeona inahitaji kusaidiwa kwa jicho la pekee. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, katika Mpango wa Mahakama wa miaka mitano ambao ni mkubwa kupita mipango yote toka uhuru, hatuwezi kusahau kabisa miundombinu mibovu katika Jimbo la Buchosa na Sengerema hasa upande wa Mahakama za Mwanzo na Mahakama za Wilaya. Pia tutazingatia kwamba Wilaya ya Sengerema ina visiwa zaidi ya 28 kitu ambacho nilikiona ni kigumu sana kukiacha hivi hivi bila kuingilia kati kwa mpango maalum wa kuwasaidia.