Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 12 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 99 2016-05-04

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA aliuliza:-
(a) Je, ni utaratibu upi uliotumika na Serikali kuzuia malipo ya 80% kwa mwezi kwa Majaji Wastaafu ambayo ni haki yao ya msingi na malipo ya mafao yao yanayotambulika kwa mujibu wa Sheria ya Majaji?
(b) Je, ni utaratibu upi unaotumika sasa kuzuia malipo hayo kwa baadhi ya Majaji?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA SHERIA NA KATIBA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Katiba ya Jamhuri ya Muungano 1977, Ibara 142(1) na (5) imeelezea kuwa malipo ya mishahara na mafao ya Jaji wa Mahakama ya Rufani na Jaji wa Mahakama Kuu yanalipwa kupitia Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali. Aidha, Sheria ya Mafao na Maslahi ya Majaji ya mwaka 2007 na Sheria ya Mafao na Hitimisho la Kazi kwa Watumishi wa Umma Na.2 ya mwaka 1999 nazo zimefafanua kuwa malipo ya mishahara na mafao ya Jaji wa Mahakama ya Rufani na wa Mahakama Kuu yatalipwa na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Fedha na Mipango hutekeleza wajibu wa kulipa 80% ya pensheni kwa Jaji aliyestaafu baada ya kupata na kuzifanyia uhakiki nyaraka zote muhimu kutoka Mahakama na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ambayo Jaji husika alichangia. Kwa Jaji Mstaafu ambaye ana stahili ya kulipwa pensheni ya kila mwezi na PSPF au Mfuko wowote aliouchangia, stahili yake ya 80% hulipwa kwa kuongeza kiwango cha fedha inayopaswa kufikia 80% ya mshahara wa Jaji aliyeko madarakani.
Mheshimiwa Naibu Spika, endapo Jaji Mstaafu hastahili kulipwa pensheni ya kila mwezi kutokana na kutotimiza sharti la kuchangia muda wa chini katika Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ambao ni kipindi cha miaka 15, asilimia 80 ya pensheni yake ya kila mwezi hulipwa na Hazina kwa asilimia 100. Malipo haya ya asilimia 80 huhuishwa kila wakati na Hazina kulingana na viwango vya mishahara ya Majaji waliopo madarakani.