Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya haraka kuhakikisha Vijiji vya Mumburu, Mkwera na Nanditi vinapata huduma za umeme kwani vipo karibu na nguzo kubwa za umeme? (b) Je, Serikali itapeleka lini umeme kwenye Zahanati za Chikundi, Mbemba na Kituo cha Afya cha Chiwale?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Mwambe nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza, kuna taarifa kwamba mkandarasi ambaye amepewa kazi ya kukamilisha miradi hii ya REA katika Mkoa wa Mtwara, hasa Wilaya ya Masasi yenye Jimbo la Ndanda pamoja na Nanyumbu ana matatizo ya kiusajili.
Je, Serikali haioni ni wakati mwafaka wa kuachana na mkandarasi huyu na kumtafuta mwingine ambaye atakamilisha kazi hii kwa wakati? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, umeme ni huduma, lakini pia umeme ni biashara. Inakuaje mji mpya unapoanzishwa watu wamekaa wanahitaji huduma ya umeme lakini hawaipati kwa wakati? Serikali mnahujumu shirika hili? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza kwa niaba ya Mheshimiwa Cecil Mwambe na swali lake la kwanza limejielekeza kwa Mkandarasi anayefanya Mradi huu wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza ambaye kwa mujibu wa jibu langu la msingi nimemtaja, JV RADI Services.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maelezo ya Mheshimiwa Mbunge, nataka nimthibitishie kwamba mkandarasi huyu siyo kwamba ana tatizo la usajili, ni utaratibu wa kawaida wa kuhakiki ambao upo ndani ya Serikali. Kuna jumla ya Wakandarasi sita katika Mradi huu wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza ambao uhakiki wao unaendelea kwa vyombo mbalimbali.
MheshimiwaMwenyekiti, kwa hiyo, naomba wakazi wa Mtwara wavute subira kwamba hivi karibuni tu uhakiki huo utakamilika na ataendelea na kazi. Sambamba na hilo, pamoja na uhakiki huo, huyu mkandarasi alipewa mkataba kwa mujibu wa taratibu, lakini pia ameanza kazi. Kuna vijiji kama vitatu Mtwara Vijijini amewasha umeme, anaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, kwa maeneo ya miji ambayo inakua, Mheshimiwa Mbunge ameeleza kwamba upatikanaji wa umeme au uunganishwaji wa miundombinu ya umeme unakuwa ni shida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge na kama ambavyo tumewasilisha bajeti yetu jana, kuna miradi mbalimbali ambayo Serikali imeona ianze kutekeleza ili kukidhi mahitaji ya umeme katika miji inayokua. Mfano, kuna mradi unaokuja peri-urban Awamu ya Kwanza utakaoanza mwaka wa fedha 2018/2019. Pia hata densification ya awamu ya pili ambayo ni kwa mikoa 11 ikiwemo Mtwara, Dodoma, Kagera, Singida, Lindi, Kilimanjaro, itaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali imeliona hilo kwa kuwa kazi ni nyingi na tumeona tuisaidie hilo liweze kuendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya haraka kuhakikisha Vijiji vya Mumburu, Mkwera na Nanditi vinapata huduma za umeme kwani vipo karibu na nguzo kubwa za umeme? (b) Je, Serikali itapeleka lini umeme kwenye Zahanati za Chikundi, Mbemba na Kituo cha Afya cha Chiwale?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kusisitiza kwamba Awamu ya Tatu ya REA ni awamu ya kuwasha Tanzania nzima na kwamba umeme utakapokwenda vijijini hakuna hata kaya itarukwa. Ni ukweli kwamba usambazaji huu unapofanyika vipo vitongoji au vijiji coverage inakuwa ni ndogo sana. Mfano Kijiji cha Gwangali kule Karatu, kati ya vitongoji vitano, ni vitongoji viwili tu ndiyo umeme umevifikia. Nini kauli ya Serikali juu ya wakandarasi hawa ambao hawazingatii maelekezo ya Serikali?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Karatu, ambaye ameuliza nini kauli ya Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu jana kupitia hotuba ya bajeti yetu ya Wizara ya Nishati, tumesema kinagaubaga kwamba mkakati wa Serikali ni kuhakikisha vijiji na vitongoji vinafikiwa na huduma ya umeme. Kwa hiyo, tumetoa rai kwa wakandarasi. Kwa mujibu wa hotuba yetu, tumesema kutokana na mpango huo na ndiyo maana kuna vijiji vya nyongeza 1,541 ambavyo tunavifanyia uhakiki. Kwa hiyo, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge, nia ya Serikali ni kufikisha umeme kadri inavyowezekana. (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya haraka kuhakikisha Vijiji vya Mumburu, Mkwera na Nanditi vinapata huduma za umeme kwani vipo karibu na nguzo kubwa za umeme? (b) Je, Serikali itapeleka lini umeme kwenye Zahanati za Chikundi, Mbemba na Kituo cha Afya cha Chiwale?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza.
Pamoja na kazi nzuri ambayo inafanywa na Wizara ya Nishati katika kusambaza umeme vijijini, lakini zipo taarifana hali halisi ndivyo ilivyo kwamba REA Awamu ya Tatu inasuasua sana kwa madai kwamba wakandarasi hawajalipwa pesa zao. Sasa ni lini Serikali itawalipa pesa zao ili wakandarasi hawa waongeze kasi ya kusambaza umeme kama ambavyo Serikali imeahidi hapa ndani ya Bunge?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na napenda nimthibitishie Mheshimiwa Nape kwamba wiki mbili zilizopita Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Benki Kuu ilifungua Letter of Credit kwa makampuni zaidi ya 18 kiasi cha shilingi bilioni 260. Naomba nilithibitishie Bunge lako tukufu kwamba kuanzia sasa miradi ile itashika kasi kwa sababu tatizo la ufunguaji wa Letter of Credit limekwisha na Benki Kuu imefanya kazi yake na ninapenda niishukuru sana. Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya haraka kuhakikisha Vijiji vya Mumburu, Mkwera na Nanditi vinapata huduma za umeme kwani vipo karibu na nguzo kubwa za umeme? (b) Je, Serikali itapeleka lini umeme kwenye Zahanati za Chikundi, Mbemba na Kituo cha Afya cha Chiwale?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mikumi ni Jimbo la kitalii na kuna wawekezaji wengi sana wamejenga mahoteli kule katika Jimbo la Mikumi katika maeneo ya Kikwalaza, Tambukareli pamoja na kule Msimba, lakini mpaka leo wanatumia majenereta na hawana umeme. Je, Serikali haioni umuhimu wa kupeleka umeme maeneo hayo ili kuwawezesha wawekezaji wetu waweze kuwekeza katika sekta hii muhimu ya utalii?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii, kama ambavyo nakumbuka naye Mheshimiwa Haule anakumbuka, Bunge lako hili hili aliuliza swali la msingi kuhusu upelekaji wa umeme katika Jimbo lake. Napenda nimthibitishie kwamba majibu tuliyotoa ya upelekaji wa umeme wa Awamu ya Tatu na kwa maeneo aliyotaja ambayo yanahusiana na masuala ya utalii, Serikali ya Awamu ya Tano italifanyia kazi. Namwomba aiunge mkono bajeti yetu leo, tuendelee kufanya kazi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya haraka kuhakikisha Vijiji vya Mumburu, Mkwera na Nanditi vinapata huduma za umeme kwani vipo karibu na nguzo kubwa za umeme? (b) Je, Serikali itapeleka lini umeme kwenye Zahanati za Chikundi, Mbemba na Kituo cha Afya cha Chiwale?

Supplementary Question 5

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Nishati alifanya ziara katika Jiji la Arusha tarehe 18 Machi na alifanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Mkonoo, Kata ya Terat na kuwaahidi hadi kufikia mwezi Aprili, umeme wa REA utakuwa umeshaanza kushughulikiwa, lakini sasa ni Mei hakuna chochote kinachoendelea, je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake kwa wananchi hawa wa Mkonoo, Kata ya Terat? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa, ni kweli Mheshimiwa Waziri alifanya ziara katika Kata hiyo ya Terat na kwa kuwa Mkoa wa Arusha Mkandarasi wake NIPO ambaye anafanya kazi vizuri alitoa maelekezo hayo na kwa kuwa mkandarasi NIPO ni mmojawapo wa Wakandarasi ambao wamefunguliwa Letter of Credit na ameagiza vifaa, ninaamini kwamba kazi itafanyika. Kwa hiyo, napenda nimwagize Mkandarasi NIPO wa Mkoa wa Arusha atekeleze agizo la Mheshimiwa Waziri na kwamba mwezi huu wa tano unaoendelea mpaka mwezi wa sita umeme uwe umewaka katika maeneo haya ambayo yameainishwa. Nampongeza sana Mheshimiwa Catherine. (Makofi)