Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 37 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 312 2018-05-25

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO (K.n.y. MHE. CECIL D. MWAMBE) aliuliza:-
(a) Je, Serikali ina mikakati gani ya haraka kuhakikisha Vijiji vya Mumburu, Mkwera na Nanditi vinapata huduma za umeme kwani vipo karibu na nguzo kubwa za umeme?
(b) Je, Serikali itapeleka lini umeme kwenye Zahanati za Chikundi, Mbemba na Kituo cha Afya cha Chiwale?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Ndanda, lenye kipengele (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, nia ya Serikali ni kuvipatia umeme vijiji vyote Tanzania Bara visivyokuwa na miundombinu ya umeme ifikapo mwezi Juni, 2021. Ili kutimiza azma hiyo, Serikali imeanza kutekeleza Mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza na jumla ya vijiji vitano vimeingizwa kwenye mradi huu unaotekelezwa na Mkandarasi aitwaye JV RADI Services, Njarita Contractors and Aguila Contractors. Vijiji hivyo ni Mwambao, Mji Mwema, Nanganga B, Tuungane na Nanditi. Wigo wa kazi katika eneo hilo ni ujenzi wa kilometa 7.16 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 na kilometa 14 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4/0.23, ufungaji wa transfoma saba na kuunganisha wateja wa awali 184. Gharama za kazi hizo ni shilingi milioni 683.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Vijiji vya Mumburu na Mkwera ni miongoni mwa vijiji 36 visivyokuwa na umeme kati ya vijiji 64 katika Jimbo la Ndanda vitakavyopatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu, mzunguko wa pili utakaotekelezwa kuanzia mwezi Julai, 2019 hadi mwezi Juni, 2021.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Zahanati ya Chikundi ina umeme tangu tarehe 25, Aprili, 2017. Aidha, Kituo cha Afya cha Chiwale kina umeme baada ya kuunganishwa wakati wa utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Pili. Vilevile Zahanati ya Mbemba itapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza unaoendelea kutekelezwa. Ahsante.