Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wananchi wa Bukoba Vijijini wanakabiliwa na tatizo kubwa la wanyama waharibifu kama vile ngedere na kadhalika na wanyama hao sasa wanavamia vijiji na kusababisha madhara kwa wananchi:- Je, Serikali ina mkakati gani madhubuti wa kuwanusuru wananchi wa Bukoba Vijijini na balaa la wanyama hao waharibifu?

Supplementary Question 1

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Serikali iko pamoja na Halmashauri ya Wilaya kudhibiti wanyama hawa waharibifu, je, Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha kuwa inawapatia vifaa vya kutosha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tunaelewa kuwa wanyama hawa ni waharibifu, je, hakuna njia nyingine ya kuwadhibiti wanyama hawa badala ya kuwauwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alfredina Apolinary Kahigi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa akishirikiana na Serikali katika kufuatilia masuala haya. Niseme tu kama nilivyokuwa nimesema kwenye swali la msingi, tumechukua hatua kadhaa katika kuhakikisha tunawadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ambayo ipo, ni kweli kabisa vifaa vya kudhibiti bado havitoshi hata hivyo tunaendelea kujipanga vizuri kuhakikisha kwamba tunapata vifaa vya kisasa vitakavyosaidia kuwadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo yote ikiwa ni pamoja na kutumia zile ndege zisizowakuwa na rubani lakini pia kufanya shughuli nyingine ambazo zitawafukuza wale wanyamapori kusudi wasilete uharibifu ule ambao umekuwa ukijitokeza katika maeneo mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, ni kweli kabisa hatupendekezi na hatushauri watu kuwaua wanyamapori, kwa sababu wanyamapori wanayo haki ya kuishi katika nchi hii kama Mungu alivyofanya uumbaji yeye mwenyewe kwamba lazima viwepo hapa duniani. Kwa hiyo, hizi ni maliasili ambazo lazima zilindwe. Hata hivyo, pale inapoonekana kwamba wamekuwa wengi tunafanya uvunaji endelevu ndipo hapo tunaweza kuwaua. Ngedere wakizidi ndiyo tunawaua otherwise tunakuwa na idadi ambayo lazima iendelee kuwepo na hatushauri viongozi wetu au wafanyakazi wetu kuwaua wanyama hao.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wananchi wa Bukoba Vijijini wanakabiliwa na tatizo kubwa la wanyama waharibifu kama vile ngedere na kadhalika na wanyama hao sasa wanavamia vijiji na kusababisha madhara kwa wananchi:- Je, Serikali ina mkakati gani madhubuti wa kuwanusuru wananchi wa Bukoba Vijijini na balaa la wanyama hao waharibifu?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wengi katika Wilaya ya Urambo wanateseka kutokana na migogoro iliyopo kwenye mapori ya hifadhi. Nichukue nafasi hii kumshukuru Naibu Waziri ambaye anajibu maswali sasa hivi alikuja kumaliza migogoro ile lakini haikuwezekana kutokana na muda mfupi uliokuwepo. Je, anatuambia nini sisi wananchi wa Urambo atakuja kumaliza migogoro iliyopo Runyeta ambako walichomewa nyumba zao na mazao yao, Tevera katika Kata ya Uyumbu na Ukondamoyo ambayo bado kuna mchuano mkubwa sana ambapo wananchi wamekosa mahali pa kulima kutokana na migogoro ya misitu?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Sitta, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza kwa jinsi ambavyo amefanya kazi nzuri ya kuhamasisha wadau mbalimbali kuhakikisha fedha zinapatikana kwa ajili ya ujenzi wa vyoo katika shule zetu. Hongera sana mama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nilishafika katika eneo lile, nilikutana na wananchi na tukajadiliana juu ya mgogoro uliopo na Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii atatembelea eneo lile ili aweze kukutana na wananchi na kuhakikisha kwamba sasa ule mgogoro ambao ulikuwepo muda mrefu unaisha mara moja. Kwa hiyo, naomba asubiri kidogo Waziri ataenda katika eneo hilo na sasa watakaa pamoja kulitafutia uvumbuzi wa kudumu tatizo hilo.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:- Wananchi wa Bukoba Vijijini wanakabiliwa na tatizo kubwa la wanyama waharibifu kama vile ngedere na kadhalika na wanyama hao sasa wanavamia vijiji na kusababisha madhara kwa wananchi:- Je, Serikali ina mkakati gani madhubuti wa kuwanusuru wananchi wa Bukoba Vijijini na balaa la wanyama hao waharibifu?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mwaka 2015/2016 wanyama wakali walipoteza maisha ya wananchi watano katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu. Hivi sasa Halmashauri ya Mbulu toka ianzishwe mwaka 2015 haina Maafisa wa Wanyamapori. Je, ni lini Serikali yetu itatusaidia kutupatia Askari wa Wanyamapori katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Issaay, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na upungufu wa wafanyakazi katika maeneo mengi ikiwemo Maafisa Wanyamapori. Katika jitihada ambazo zinafanyika sasa hivi tumeweka kwenye bajeti inayokuja kuangalia kama tunaweza kupata wafanyakazi wachache ambao tutawasambaza katika wilaya mbalimbali hapa nchini. Naomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira hilo likikamilika tutafikiria Wilaya ya Mbulu ili waweze kupata wafanyakazi hao.