Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga theatre pamoja na vifaa vyake vya upasuaji katika Wilaya ya Namtumbo, Mji Mdogo wa Lusewa. Ahadi hii ni ya muda mrefu na wananchi wamekuwa wakiteseka kutokana na ukosefu wa huduma hiyo jambo ambalo limesababisha vifo hasa kwa akinamama wajawazito na watoto:- a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo? b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba ya Daktari katika Kituo cha Afya cha Lusewa?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Serikali ambayo kimsingi yameacha kujibu kipengele (b), sasa naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Lusewa ni Mji Mdogo ambao sasa hivi umeshapandishwa hadhi na kuwa Mji Mdogo. Ni eneo ambalo lina wakazi wengi sana. Kutoka Lusewa kwenda Nalasi kuna umbali wa kilometa 150 na kutoka Lusewa kwenda Songea Mjini kwenye hospitali ya rufaa kuna kilometa 150. Wanawake wenzangu wa eneo hilo la Lusewa katika Mji Mdogo wamekuwa wakipata shida sana hasa kwenye suala la usalama wao wa uzazi na usalama wa mama na mtoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, wanawake na watoto wamekuwa wakipoteza maisha na siku moja nilisimama hapa katika Bunge lako Tukufu nilionesha hisia zangu kwamba imefika mahali sasa kumtoa mwanamke kwenye Kituo hiki cha Lusewa ambacho hakina theatre kumpeleka Nalasi kilometa 150, gari la kubebea hao wagonjwa hakuna, wakati mwingine ni mabovu. Naomba Serikali inipe majibu ya kina ni lini itakamilisha ujenzi wa kituo hiki cha afya pamoja na kuweka hii theatre ambayo itawasaidia akinamama hawa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, anyway siyo swali lakini ni ombi, niseme kwamba, je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuongozana nami pamoja na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Mkurugenzi wa Namtumbo na DMO wa Namtumbo ili aende akaone mwenyewe kwa macho jinsi ambavyo wanawake wanavyopata tabu na watoto wanapoteza maisha katika maeneo yale? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi kwamba ujenzi wa kituo kile cha afya umekamilika isipokuwa chumba cha upasuaji kilichobaki ni sakafu peke yake. Naomba nitumie fursa hii kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ahakikishe kwamba katika vyanzo vyake vya mapato kwa kushirikiana na wananchi kazi ya kumalizia sakafu iweze kukamilika ili wananchi waendelee kupata huduma badala ya kusubiri mpaka hicho kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020. Naamini kabisa katika vyanzo vyao vya mapato wakijibana wanaweza kumalizia kabisa suala zima la sakafu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameomba mimi kuambatana na Waheshimiwa Wabunge wa maeneo hayo. Naomba nimhakikishie, katika maeneo ambayo nina deni la kwenda kujionea mimi mwenyewe ni pamoja na Mkoa wa Mtwara lakini nikitoka Mtwara nitakuwa naenda Ruvuma halafu nitakwenda Njombe. Ilikuwa niende kwa bahati mbaya nikawa nimepatwa na msiba. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira. (Makofi)

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga theatre pamoja na vifaa vyake vya upasuaji katika Wilaya ya Namtumbo, Mji Mdogo wa Lusewa. Ahadi hii ni ya muda mrefu na wananchi wamekuwa wakiteseka kutokana na ukosefu wa huduma hiyo jambo ambalo limesababisha vifo hasa kwa akinamama wajawazito na watoto:- a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo? b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba ya Daktari katika Kituo cha Afya cha Lusewa?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ahadi ni deni na kwa vyovyote vile Ilani hutekelezwa ndani ya miaka mitano, imekuwa ni kawaida kwamba Ilani ya Chama cha Mapinduzi mara nyingi haitekelezwi siyo tu kwenye masuala ya afya ni pamoja na barabara na elimu. Nataka kupata kauli ya Serikali, je, hizi ahadi zao hasa za Marais zinakuwa ni za kuwadanganya watu? Pia ni lini sasa ahadi zote kuanzia zile za Mheshimiwa Mkapa…

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili ambalo linaulizwa leo halina tofauti kabisa na ambalo aliuliza Mheshimiwa Sophia Mwakagenda kuhusiana na ahadi za wagombea Urais na utekelezaji wa Ilani ya CCM. Katika majibu yangu ambayo nilitoa siku ile nilieleza kwamba ahadi zimekuwa zikitekelezwa na Waheshimiwa Wabunge wengi wamekuwa wakishukuru jinsi ambavyo ahadi zinatekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ahadi za wagombea Urais ndiyo mkataba wao na wananchi na wananchi wamekuwa wakiwapigia kura kwa ku-base kwenye hizo ahadi ambazo zinatolewa na Ilani ya CCM inatekelezwa ndani ya miaka mitano.
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru kwa sababu amekuwa anafuatilia utekelezaji wa Ilani ya CCM na yeye mwenyewe anaamini kwamba tunatekeleza. Sasa amesema haitekelezwi, nadhani hapo atakuwa amepitiwa. Akatazame yale tuliyoahidi mangapi tumetekeleza, suala zima la afya yeye mwenyewe ni shuhuda na juzi tulikuwa tunaongea naye kuhusiana na barabara ya kule kwake na kazi imeshaanza kufanyika, kwa hiyo tunatekeleza. (Makofi)

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga theatre pamoja na vifaa vyake vya upasuaji katika Wilaya ya Namtumbo, Mji Mdogo wa Lusewa. Ahadi hii ni ya muda mrefu na wananchi wamekuwa wakiteseka kutokana na ukosefu wa huduma hiyo jambo ambalo limesababisha vifo hasa kwa akinamama wajawazito na watoto:- a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo? b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba ya Daktari katika Kituo cha Afya cha Lusewa?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali moja la nyongeza; Kituo cha Afya Kibiti kimezidiwa, je, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa ikizingatia pale hakuna X-ray, nyumba za wagonjwa na maabara ya uhakika?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ungando, Mwenyekiti wa Wandengereko ambaye kwa mara ya kwanza amenipandisha boti nikaenda Delta, sehemu ambayo unaambiwa kwamba ikifika muda fulani maji yakikauka inabidi usibiri saa nne. Nimefika kule na naomba nimpongeze jinsi ambavyo anapigania wananchi wa Jimbo lake la Kibiti. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri kazi ambayo tulienda kusimamia sasa inakwenda vizuri. Kuna mambo ya hovyo yalikuwa yanafanyika katika ujenzi wa kituo kile cha afya lakini hata jana nilikuwa naongea na Mwenyekiti wa CCM ambaye alikuwa Mbunge, Ndugu Jabir Marombwa amenihakikishia ujenzi unakwenda vizuri. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, eneo hilo ambalo hakuna X-ray tayari tumeshapeleka pesa MSD kwa ajili ya vifaa, kwa sababu tunataka vituo vya afya vikamilike kwa kuwa na vifaa pamoja na wataalam ili vitoe huduma iliyokusudiwa kwa wananchi. (Makofi)

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga theatre pamoja na vifaa vyake vya upasuaji katika Wilaya ya Namtumbo, Mji Mdogo wa Lusewa. Ahadi hii ni ya muda mrefu na wananchi wamekuwa wakiteseka kutokana na ukosefu wa huduma hiyo jambo ambalo limesababisha vifo hasa kwa akinamama wajawazito na watoto:- a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo? b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba ya Daktari katika Kituo cha Afya cha Lusewa?

Supplementary Question 4

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na upungufu wa watumishi katika sekta ya afya lakini maslahi ya watumishi katika sekta ya afya yamekuwa duni hasa on call allowance ambayo Serikali kwa muda mrefu sasa haijapeleka fedha hizo katika OC. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha hizo ili kusaidia Madaktari kufanya kazi zao kwa ufanisi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, hivi leo ninavyoongea katika maeneo yote ambayo kumekuwa na hamasa kubwa wananchi wakajiunga na CHF, hakuna tatizo la Madaktari kulipwa on call allowance. Akitaka kuchukua mfano, nimeenda Tanga pale sasa hivi katika hizi pesa ambazo wananchi wanachangia kwa kujiunga na Bima ya Afya, kulipana on call allowance si tatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Naomba Mheshimiwa Mbunge ahamasishe maeneo ya kwake wananchi wajiunge na Bima ya Afya na michango ile ambayo inatolewa ya ‘Papo kwa Papo, Tele kwa Tele’ hakika katika maeneo yote ambayo nimepita tangu utaratibu huu umeanza, kulipana on call allowance siyo tatizo tena.