Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 59 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 497 2018-06-27

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:-
Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kujenga theatre pamoja na vifaa vyake vya upasuaji katika Wilaya ya Namtumbo, Mji Mdogo wa Lusewa. Ahadi hii ni ya muda mrefu na wananchi wamekuwa wakiteseka kutokana na ukosefu wa huduma hiyo jambo ambalo limesababisha vifo hasa kwa akinamama wajawazito na watoto:-
a) Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi huo?
b) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba ya Daktari katika Kituo cha Afya cha Lusewa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa jengo la upasuaji katika Kituo cha Afya Lusewa ulianza mwaka 2015. Ujenzi uliendelea katika mwaka wa fedha 2017/2018 ambapo fedha zilipelekwa moja kwa moja kwenye akaunti ya kituo. Jengo la OPD limekamilika isipokuwa sakafu ya chumba cha upasuaji. Kituo hicho kitawekwa katika kipaumbele na kutengewa bajeti katika mwaka wa fedha 2019/2020 ili kukamilisha ujenzi unaoendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, ili kuboresha huduma za afya kwa mama na mtoto, Serikali imeweka kipaumbele na kutoa jumla ya shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya ukarabati wa vituo vya afya nane katika Mkoa wa Ruvuma ambapo kati ya fedha hizo, shilingi milioni 900 zimetolewa kwa vituo viwili vya afya vilivyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ambavyo ni Kituo cha Afya Msakale na Matemanga. Vituo vingine vilivyopokea fedha katika Mkoa wa Ruvuma ni Kalembo (shilingi milioni 500), Mkili (shilingi 400), Namtumbo (shilingi milioni 400), Madaba (shilingi milioni 400), Mahukuru (shilingi milioni 500) na Mchangimbole (shilingi milioni 500).
Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati huu wa Serikali unalenga kuimarisha huduma za dharura na upasuaji kwa mama wajawazito.