Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi katika Hifadhi ya Wanyamapori Selous-Kilwa umechukua nafasi kubwa kati ya Serikali na wananchi wanaoishi karibu na hifadhi hiyo. Mpaka halali haujulikani kwani mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu na mwaka 2010 mpaka huo ulisongezwa mpaka Bwawa la Kilurumila, Kijiji cha Kikulyungu. Je, Serikali ipo tayari kuhakiki eneo hilo ili kutatua mgogoro uliopo kati yake na wananchi wa Kijiji cha Kihurumile?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu haya ambayo ameyatoa japokuwa hayaoneshi dhamira ya dhati ya kutaka kumaliza mgogoro huo. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, mgogoro huu umekuwa wa muda mrefu sana, lakini kwa majibu ya Serikali hayakuonesha hapa ni lini watakutana na viongozi wa Mkoa ili kumaliza huu mgogoro. Kwa sababu umesema tu watakaa lakini haisemi ni lini. Kwa sababu huu mgogoro ni wa muda mrefu kwa hiyo, ningeomba Serikali ituambie ni lini watadhamiria kumaliza huu mgogoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali langu la pili, kuna mgogoro pia kwenye Serikali ya Wilaya ya Kilwa na Wizara kuhusiana na mpaka huu wa Selous. Kwa hiyo, nayo Mheshimiwa Waziri ningependa aniambie ni lini mgogoro huu watamaliza ili kuepukana na vurugu ambazo zinaweza zikatokea katika kugombania mipaka hii katika maeneo haya?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hi kumpongeza sana kwa sababu amekuwa ni mdau mzuri sana wa mambo ya utalii katika eneo la kusini, kwa kweli tutaendelea kushirikiana naye. Sasa kuhusu lini tutakutana naomba nimhakikishie tu kwamba kati ya mwezi wa saba na wa tisa kabla ya Bunge la mwezi tisa tutafanya jitihada za kuhakikisha kwamba tunakutana na viongozi wa Lindi na tutashughulikia migogoro yote inayohusiana na hilo Pori la Akiba la Selous.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi katika Hifadhi ya Wanyamapori Selous-Kilwa umechukua nafasi kubwa kati ya Serikali na wananchi wanaoishi karibu na hifadhi hiyo. Mpaka halali haujulikani kwani mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu na mwaka 2010 mpaka huo ulisongezwa mpaka Bwawa la Kilurumila, Kijiji cha Kikulyungu. Je, Serikali ipo tayari kuhakiki eneo hilo ili kutatua mgogoro uliopo kati yake na wananchi wa Kijiji cha Kihurumile?

Supplementary Question 2

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini naomba niulize swali kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo migogoro inayoendelea baina ya vijiji vyetu na hifadhi zetu, ikiwemo Hifadhi hiyo ya Selous ambayo muuliza swali ameizungumza, lakini pia ipo migogoro baina ya kijiji na kijiji, hii inapelekea wananchi wengi kukosa amani.
Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kumaliza migogoro hii katika nchi yetu ili wananchi waendelee kuishi kwa amani? Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto, kumekuwa na migogoro mbalimbali katika maeneo mbalimbali yanayopakana na hifadhi. Lakini naomba nitumie nafasi hii kumueleza Mheshimiwa Mbunge kwamba kuanzia mwaka wa fedha 2018/2019 yaani Julai, Wizara kwa kushirikiana na taasisi zetu za Hifadhi za Taifa tutahakikisha kwamba vijiji vyote vinavyozunguka maeneo ya hifadhi vinapimiwa na vinaondokana na matatizo ambayo yapo katika yale maeneo. Kwa sababu tumetenga fedha kwa ajili ya hiyo kazi kwa hiyo vijiji vyote vitapitiwa.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi katika Hifadhi ya Wanyamapori Selous-Kilwa umechukua nafasi kubwa kati ya Serikali na wananchi wanaoishi karibu na hifadhi hiyo. Mpaka halali haujulikani kwani mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu na mwaka 2010 mpaka huo ulisongezwa mpaka Bwawa la Kilurumila, Kijiji cha Kikulyungu. Je, Serikali ipo tayari kuhakiki eneo hilo ili kutatua mgogoro uliopo kati yake na wananchi wa Kijiji cha Kihurumile?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyotajwa na Mheshimiwa Waziri kwamba, ndiyo vinavyochangia katika Wilaya ya Liwale kwa Selous, vijiji hivi ndivyo vilivyoanzisha mgogoro kwa sababu vijiji hivi vimepakana na Selous kwa Mto wa Matandu. Kwa nini Kikulyungu peke yake ndio ambayo imeonekana kwamba imeondoka Matandu na ndio maana wanakijiji Wakikulyungu waligoma. Sasa Mheshimiwa Waziri ninachotaka kujua je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kufuatana na Mheshimiwa Waziri wa Ardhi muende mkatafsiri GN ambayo inaitambua Pori la Akiba la Selous ukiachana na hii tangazo la mwaka 1974?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba tuko tayari kuongozana na Mheshimiwa Waziri pamoja na viongozi wengine wa Mkoa wa Lindi ili tushughulikie migogoro yote inayohusu mpaka wetu kule. (Makofi)

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi katika Hifadhi ya Wanyamapori Selous-Kilwa umechukua nafasi kubwa kati ya Serikali na wananchi wanaoishi karibu na hifadhi hiyo. Mpaka halali haujulikani kwani mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu na mwaka 2010 mpaka huo ulisongezwa mpaka Bwawa la Kilurumila, Kijiji cha Kikulyungu. Je, Serikali ipo tayari kuhakiki eneo hilo ili kutatua mgogoro uliopo kati yake na wananchi wa Kijiji cha Kihurumile?

Supplementary Question 4

MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nilitaka nimuulize Mheshimiwa Waziri pale Segerea kuna pori moja linaitwa Msitu wa Nyuki, walikuwa wanafuga nyuki zamani lakini naona Wizara imeshaachana na huo mpango wa kufuga nyuki.
Sasa Wizara ina mpango gani na hilo pori maana yake wameliacha tu, na kama hawana mpango nalo kwa nini wasitupe sisi Manispaa ya Ilala ili tuweze kulitumia katika matumizi ya soko na mambo mengine ya huduma za kijamii? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba tuna msitu katika lile eneo ambalo lilikuwa linatumika kwa ajili ya kufuga nyuki, lakini si kwamba lile pori tumeliacha tu, kuliacha tu bado linaendelea kuhifadhi ule uoto wa asili.
Kwa hiyo, bado ni pori linalotambulika vizuri kabisa na bado tutaendeleza jitihada za kufuga, lakini pia inasaidia sana katika kuweza kupunguza carbon dioxide ambayo inatokea katika viwanda mbalimbali pale Dar es Salaam. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lile eneo tutaendelea kulihifadhi na litaendelea kuhifadhia na kuendelezwa.