Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Kampuni ya Utafiti wa Gesi na Mafuta imeanza kazi kubwa ya utafiti wa mafuta na gesi katika eneo la Mng’ongo, Kijiji cha Fukayosi, Kata ya Fukayosi, Wilaya ya Bagamoyo:- Je, ni nini matokeo ya utafiti huo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu haya ambayo ametupa nina maswali mawili ya nyongeza.
Mhshimiwa Spika, kwanza, katika kipindi hichohicho kampuni ya Dodsal imefanya utafiti wa gesi na mafuta katika Kata ya Vigwaza, Wilaya ya Bagamoyo. Napenda kujua nini matokeo ya utafiti huo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, napenda kujua ni maeneo gani katika Mkoa wa Pwani ambapo gesi imegundulika kwa kiwango cha kibiashara?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Jumanne Shukuru Kawambwa. Namshukuru sana ameuliza swali katika Kata yetu ya Fukayosi.
Mheshimiwa Spika, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli Kampuni hii ilifanya utafiti pia katika maeneo ya Vigwaza, Kwala na Ruvu. Kazi inayoendelea sasa hivi ni kukusanya data na kuzichakata zile takwimu za mitetemo ambazo zinaitwa 3D. Kwa hiyo, kazi hiyo inaendelea ili kubaini kiwango cha gesi asilia kilichopo katika mashapo ambayo gesi imegundulika katika maeneno hayo.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameuliza ni maeneo gani katika Mkoa wa Pwani mpaka sasa gesi imegundulia. Kwa kweli ni maeneo hayo kama ambavyo nimesema katika jibu hili la nyongeza, ni Kwala, Ruvu na Vigwaza ambapo utafiti unaendelea. Sasa hivi data ambazo wanazikusanya za mitetemo hiyo ya 3D wanaendelea kuzifanyia michakato ili kubaini kiwango cha gesi na kuweza kutathmini kama kinafaa katika vigezo mbalimbali vya kiuchumi. Nakushukuru sana.

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Kampuni ya Utafiti wa Gesi na Mafuta imeanza kazi kubwa ya utafiti wa mafuta na gesi katika eneo la Mng’ongo, Kijiji cha Fukayosi, Kata ya Fukayosi, Wilaya ya Bagamoyo:- Je, ni nini matokeo ya utafiti huo?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali imekuwa na utaratibu wa kupeleka wanafunzi katika vyuo vya nchi za nje kwa ajili ya kupata utaalam kwenye masuala ya gesi na mafuta. Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanafunzi hawa baada ya masomo wanapata ajira kwenye makampuni haya ambayo yanafanya tafiti kwenye Taifa letu ili waweze kuonyesha uwezo wao, experience yao na uzalendo wao katika makampuni ya utafiti? Ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la nyongeza. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Kishoa linalohusu masuala ya namna gani Serikali imejipanga kutumia utaalam wa vijana ambao wamekuwa wakipelekwa nchi mbalimbali kupata mafunzo katika eneo la mafuta na gesi. Ni kweli kwamba utaratibu huo upo na hata mwaka huu wa fedha unaoendelea tumepokea nafasi 20 kutoka katika nchi ya China kwa ajili ya kupeleka vijana wetu.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa utelekezaji wa miradi ya gesi na mafuta unayoendana na ubia baina ya Taasisi yetu ya TPDC na kampuni hizo ya kimataifa, ni wazi kabisa kwamba mpango wa Serikali ni kuona vijana wale wakihitimu wanafanya kazi katika maeneo haya. Kwa vyovyote vile, kwa kuwa baada ya kuhitimu wanakuwa wamepata teknolojia na wanatosha katika mazingira hayo, wengi wamekuwa wakipata ajira katika kampuni hizi za kimataifa zinazofanya utafiti ndani ya nchi yetu lakini Serikali itaendelea na utaratibu huo. Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Spika, naomba niongeze majibu kidogo kwenye suala hili la msingi sana la kuweza kuwawezesha Watanzania kushiriki katika uchumi unaojengwa kwenye nchi yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Spika, baada ya kuona kwamba mageuzi makubwa ya kiuchumi yanafanyika na hasa uwepo wa miradi mikubwa ya kimkakati katika nchi yetu, Serikali imefanya kwa makusudi marekebisho ya sheria mbalimbali, lakini vilevile imetunga kanuni mbalimbali za kuhakikisha Watanzania ambao wana uwezo na weledi katika sekta hizo wanapewa kipaumbele cha ajira kwenye maeneo husika.
Mheshimiwa Spika, suala hili limeshafanikiwa, kanuni zimeshatengenezwa kwenye suala la mafuta na gesi na wenzetu wa Wizara ya Madini wameshatengeneza kanuni za kuhakikisha Watanzania wanaajirika kwenye maeneo hayo. Vilevile Ofisi ya Waziri Mkuu inatengeneza sasa mfumo mzuri wa local content wa kuhakikisha bidhaa na huduma za Watanzania zinaweza kutumika na zikashiriki katika ujenzi wa uchumi wetu kupitia miradi mikubwa ya kimkakati katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:- Kampuni ya Utafiti wa Gesi na Mafuta imeanza kazi kubwa ya utafiti wa mafuta na gesi katika eneo la Mng’ongo, Kijiji cha Fukayosi, Kata ya Fukayosi, Wilaya ya Bagamoyo:- Je, ni nini matokeo ya utafiti huo?

Supplementary Question 3

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, ili kuondokana na uharibifu wa mazingira kwa kukata miti hovyo ikiwemo matumizi ya nguzo za umeme za miti. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kutumia nguzo za chuma badala ya nguzo za miti katika kusambaza umeme vijijini na mijini? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mndolwa. Ni kweli kuna mpango huo wa kuhama kutoka kwenye matumizi ya nguzo zinazotokana na miti, na kwenda nguzo zinazotokana na zege.
Mheshimiwa Spika, kwanza Shirika letu la TANESCO limeunda kampuni tanzu kwa ajili ya kuzalisha nguzo za zege. Pili kama Wizara pia tumehamasisha wadau wa ndani kuanzisha viwanda vya kutengeneza nguzo za zege na tayari kuna viwanda Bagamoyo, Kibaha na Mbeya na hiki nilikitembelea.
Mheshimiwa Spika, kinachofuata sasa ni taratibu za manunuzi, tumewaelekeza TANESCO kwamba miradi inayoendelea ya umeme vijijini kupitia REA na kupitia hata miradi yao, tuanze kuhama kutoka kwenye nguzo hizi za miti ambazo zinadumu kwa muda mfupi sana ndani ya miaka mitano, sita wakati hizi nguzo za zege zinaweza kudumu zaidi ya miaka 20 na kuendelea. Kwa hiyo, ni wazi tutakapotimiza azma yetu ya kutumia nguzo za zege tuta-save pesa nyingi zinazotumika kwenye ukarabati wa nguzo hizi za kawaida ambazo zinachukua muda mfupi na zinaoza. Nakushukuru.