Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 48 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 411 2018-06-11

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-
Kampuni ya Utafiti wa Gesi na Mafuta imeanza kazi kubwa ya utafiti wa mafuta na gesi katika eneo la Mng’ongo, Kijiji cha Fukayosi, Kata ya Fukayosi, Wilaya ya Bagamoyo:- Je, ni nini matokeo ya utafiti huo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Kampuni ya Gesi na Mafuta iitwayo Dodsal Hydrocarbons & Power (Tanzania) kutoka Falme za Kiarabu inaendelea na utafiti wa mafuta na gesi katika eneo la Mng’ongo katika Kijiji cha Fukayosi, Kata ya Fukayosi, Wilaya ya Bagamoyo.
Mheshimiwa Spika, kupitia utafiti huo, Kampuni ya Dodsal Hydrocarbons & Power ilifanikisha kuchimba kisima cha utafiti chenye urefu wa mita 3,866 kiitwacho Mtini-1. Kisima hicho kilianza kuchimbwa tarehe 8 Mei, 2015 na kufungwa tarehe 20 Julai 2015. Matokeo ya utafiti katika kisima hiki ni kwamba haikugundulika gesi ya kutosha kukidhi matakwa ya kiuchumi ingawaje kuna viashiria vya gesi kidogo vilivyoonekana wakati wa uchimbaji katika mashapo ya miamba ya eneo hilo. Ahsante sana.