Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA (K.n.y. MHE. MARIA N. KANGOYE) aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko mengi juu ya wananchi wanyonge hususani wanawake wajane na yatima kudhulumiwa ardhi hususani maeneo ya vijijini:- Je, ni lini Serikali itaweka mikakati ya Kiwilaya ili kuwasaidia wananchi hao?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kumuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Mkoani Mwanza kuna eneo la wananchi limechukuliwa kwa ajili ya matumizi ya Ikulu ndogo ikiwemo na lile eneo lenye mradi wa UWT. Napenda kujua sasa ni lini Serikali itawafidia wananchi hao pamoja na taasisi ambazo maeneo yao yamechukuliwa ikizingatiwa wananchi hao wamesitisha shughuli za maendeleo kwa ajili ya kupisha zoezi hilo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili eneo la Bugosi, Kata ya Nyandoto, Wilayani Tarime, kuna eneo la wananchi limechukuliwa na Jeshi takribani miaka mitano ama zaidi. Napenda kujua sasa ni lini Serikali itawafidia wananchi hao ilhali tathmini ya eneo hilo tayari ilishafanyika? Ahsante. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mchafu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, katika eneo ambalo Mheshimiwa Mbunge analitaja ingekuwa vizuri tukapata fursa ya kwanza kujua chanzo cha tatizo kwa kujiridhisha ili pande zote tujue nini kinatakiwa kifanyike ili haki iweze kutendeka. Ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba hakuna kipande cha ardhi cha mwananchi kitachukuliwa bila kupata fidia. Kwa hiyo, katika hilo eneo ambalo amelitaja ni vizuri tukajiridhisha hasa tatizo ni nini ili wananchi kama wanastahili fidia waweze kupata.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili anaelezea eneo ambalo liko Tarime anasema kwamba eneo hilo limechukuliwa na Jeshi. Itakuwa ni ngumu sana unless kama tumejiridhisha kwa sababu Jeshi maeneo ambayo imekuwa ikitwaa ardhi kuna utaratibu ambao unawekwa juu ya fidia na fidia imekuwa ikitolewa. Katika hili ambalo ni jipya ni vizuri Mheshimiwa Mbunge akatoa fursa Serikali tukajiridhisha hasa nini ambacho kimetokea mpaka Jeshi ikaonekana limetwaa eneo hilo bila fidia. Maana inawezekana wananchi ndiyo wamelifuata Jeshi au Jeshi limekuja baada ya eneo la wananchi. Kwa hiyo, ni vizuri kutizama pande zote mbili ili kuweza kutoa majibu ambayo ni sahihi.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA (K.n.y. MHE. MARIA N. KANGOYE) aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko mengi juu ya wananchi wanyonge hususani wanawake wajane na yatima kudhulumiwa ardhi hususani maeneo ya vijijini:- Je, ni lini Serikali itaweka mikakati ya Kiwilaya ili kuwasaidia wananchi hao?

Supplementary Question 2

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, haya matatizo ya ardhi yanasaidiwa na Mabaraza yetu ya Kata na Wilaya kufanya kazi, lakini tuna tatizo kubwa kwa Wenyeviti wetu wa Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya kuhudumia Wilaya zaidi ya mbili au tatu na wakati mwingine Wenyeviti hao mikataba yao imekuwa ikiisha lakini haiwi renewed kwa wakati. Kwa mfano, Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Wilaya ya Babati ambaye anahudumia Mbulu, Hanang na maeneo mengine mkataba wake umeisha muda mrefu na wananchi wanapata shida. Naomba nifahamu, ni lini mkataba wa Mwenyekiti huyu na Wenyeviti wengine mta-renew ili wananchi wapate haki zao kwa wakati? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gekul, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, itakuwa si vizuri sana tukaliongea suala hili in blanket maana kuna kesi na kesi si kwamba Tanzania nzima mikataba haijakuwa renewed. Ingekuwa vizuri baada ya kumaliza kipindi hiki tukajua exactly ni nini ambacho kimetokea kwa kesi yake ambayo ameisema na ingekuwa ni vizuri na mimi nikalijua ili tujue namna nzuri ya kuweza kulitatua ili wananchi hao waendelee kuhudumiwa kama ipasavyo.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA (K.n.y. MHE. MARIA N. KANGOYE) aliuliza:- Kumekuwa na malalamiko mengi juu ya wananchi wanyonge hususani wanawake wajane na yatima kudhulumiwa ardhi hususani maeneo ya vijijini:- Je, ni lini Serikali itaweka mikakati ya Kiwilaya ili kuwasaidia wananchi hao?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, panapotokea migogoro hiyo basi wananchi wengi wanakimbilia kupata suluhu katika Mabaraza yetu ya Ardhi ya Kata, lakini uwezeshwaji ili kuwepo na ufanisi wa Mabaraza hayo umekuwa ukisuasua. Mabaraza haya yanategemea faini za wateja wake ili yaweze kujiendesha na halmashauri imekuwa haisaidii. Je, ni lini sasa Serikali itatia mkazo wa kuwezesha Mabaraza haya ili ufanisi uweze kupatikana?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Paresso, nilitaka kusema Gekul maana wakati mwingine wanafanana, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba uanzishwaji wa Mabaraza ya Ardhi ilikuwa ni kwa ajili ya kusaidia wananchi na hasa katika maeno ambayo wale wajumbe wanayafahamu vizuri kulikoni kwenda kwenye mambo ya kisheria. Tunachotarajia kwanza ni wao kwenda kubaini na kuweza kusuluhisha.
Mheshimiwa Spika, pia ni ukweli usiopingika kwamba baadhi ya Mabaraza wamekuwa wakitumia zile tozo ambazo wanatoza wananchi kama chanzo na wakati mwingine kumekuwa mpaka hata haki kutotendeka. Ni vizuri tukalitizama kwa ujumla wake, maeneo mengine wanafanya vizuri, katika maeneo ambayo hawafanyi vizuri na hasa kwa kuanzia wale wajumbe ambao wanachaguliwa kuwa katika lile Baraza, katika maeneo ambayo haki imetendeka wamekuwa wakifanya vizuri sana lakini maeneo mengine lazima tukubaliane kwamba kumekuwa na shida ni vizuri tukalitizama kwa ujumla wake ili tukafanya revision namna nzuri ya kuweza kuenenda na suala hili.