Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 48 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 408 2018-06-11

Name

Maria Ndilla Kangoye

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA (K.n.y. MHE. MARIA N. KANGOYE) aliuliza:-
Kumekuwa na malalamiko mengi juu ya wananchi wanyonge hususani wanawake wajane na yatima kudhulumiwa ardhi hususani maeneo ya vijijini:-
Je, ni lini Serikali itaweka mikakati ya Kiwilaya ili kuwasaidia wananchi hao?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maria Ndilla Kangoye, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikishughulikia migogoro ya ardhi vijijini katika ngazi mbalimbali kuanzia ngazi ya kijiji hadi ngazi ya Wizara. Migogoro inayopokelewa kutoka maeneo mbalimbali inahusu mirathi inayowagusa wajane na yatima katika maeneo ya vijijini, madai ya fidia ya fedha, viwanja/maeneo/mashamba, mwingiliano wa mipaka ya mashamba/viwanja, uvamizi wa wananchi katika maeneo ya taasisi za umma, taasisi kuingilia maeneo ya wananchi, migogoro baina ya wananchi na wawekezaji na migogoro ya wakulima na wafugaji.
Mheshimiwa Spika, mikakati ya Serikali katika kuipatia ufumbuzi migogoro ya aina hiyo ni pamoja na kuanzisha Dawati Maalum la kusikiliza na kusaidia kutatua malalamiko ya ardhi yanayowasilishwa na wananchi. Dawati hilo pamoja na mambo mengine, linabainisha siku maalum za kupokea na kusikiliza malalamiko au kero hizo. Aidha, Serikali imeimarisha utendaji wa Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji, Kata na Wilaya kwa kuelekeza kuwa uteuzi wa wajumbe wa Mabaraza hayo unakuwa wa uwiano sawia kwa kuzingatia uwepo wa uwakilishi wa wanawake.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhimiza kuandaliwa kwa mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji na wilaya (land use plans) ili kudhibiti mwingiliano wa matumizi ya ardhi. Aidha, ipo mikakati ya kurasimisha makazi kwenye vijiji na miji inayoondoa migogoro ya ardhi na kuinua kipato cha wananchi kwa kuwatayarishia hatimiliki ambazo hutumika kama dhamana katika kuomba mikopo kwenye taasisi za fedha.