Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PULINE P. GEKUL aliuliza:- Vijiji vya Imbilili, Hitimi na Managha katika Jimbo la Babati Mjini havina mawasiliano ya simu. Je, ni lini Serikali itavipa vijiji hivyo minara ya mitandao ya simu?

Supplementary Question 1

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza nimuambie tu Mheshimiwa Waziri hatuna kata ya singena tuna kata ya Singe. Lakini pia swali langu la msingi niliuliza vijiji vitatu ikiwemo Kijiji cha Chemchem Kata ya Mutuka ambayo pia haina mawasiliano.
Mheshimiwa Waziri swali la kwanza kama Halotel wameshindwa kwa nini sasa Wizara yako isifuatilie Kampuni nyingine weather Airtel au Vodacom waje waweke minara hiyo kwasababu mazungumzo haya ya Halotel ni tangu mwaka jana na hakuna kazi inayofanyika na hivi vijiji havina mawasiliano. Kwa nini usifuatilie hilo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili Serikali miaka iliyopita mwaka juzi na mwaka jana wali-centralize makusanyo yanayotokana na makampuni haya ya simu ya service levy mwanzo halmashauri zilikuwa zinalipwa moja kwa moja tulikuwa tunakusanya Halmashauri lakini Serikali ilivyo-centralize makusanyo hayo walisema watatuletea kwenye Halmashauri zetu hadi hivi ninavyoongea Halmashauri zetu hawapati service levy.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba ni lini Serikali watarudisha makusanyo hayo kwenye Halmashauri zetu maana wao ndio wanakusanya sasa halmashauri hatukusanyi?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jibu langu la msingi nimemuelekeza Mheshimiwa Gekul kwamba tumeunda timu ya wataalam kuchunguza minara yote ya simu wala sio ya kampuni moja wapo ya Halotel au Tigo au Vodacom kuangalia uhakika wa mawasiliano kwa maeneo husika ambako imewekwa minara hiyo. Kwa hiyo, hii timu itakapotuletea taarifa tutaweza kujua tufanye vitu gani kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanapata mawasiliano ya kutosha. Namshauri Mheshimiwa Mbunge awe mvumilivu hiyo timu itatuletea majibu ambako tutaweza kupata mahala pa kuanzia kufanyia kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala lake la pili kuhusu service levy haya masuala bado kwanza yanaanzia kwenye Halmashauri zetu ambapo sisi Wabunge ni Madiwani huwa mapato yakipatikana huwa yanapelekwa accordingly kutokana na mapatano kati ya halmashauri zetu na makampuni ya simu.