Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 45 Works, Transport and Communication Wizara ya Nishati 388 2018-06-06

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PULINE P. GEKUL aliuliza:-
Vijiji vya Imbilili, Hitimi na Managha katika Jimbo la Babati Mjini havina mawasiliano ya simu. Je, ni lini Serikali itavipa vijiji hivyo minara ya mitandao ya simu?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano napenda kujibu swali la Mheshimiwa Pauline Gekul, Mbunge wa Babati mjini kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote ilifanya tathmini katika Kijiji cha Imbilili kata ya Singino, Himiti Kata ya Bonga pamoja na Kijiji cha Managha Kata ya Singena kwa kuangalia hali halisi ya mawasiliano pamoja na idadi ya wakazi. Vijiji hivyo viliingizwa katika orodha ya vijiji vinavyohitaji huduma ya mawasiliano. Vijiji hivyo vyote viliweza kupelekewa mawasiliano kupitia Kampuni ya Viettel ambayo inamilikiwa kampuni ya Halotel kwa ajili ya mawasiliano. Hata hivyo ninazo taarifa kwamba minara hiyo haifanyi kazi vizuri sana na nimetuma timu ya wataalamu kwenda kuhakikisha kwamba kuna tatizo gani katika minara hiyo kwa ajili ya kuhakikisha wanapata mawasilino wananchi wa eneo hilo.