Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni lini tatizo la kukatika mara kwa mara kwa umeme katika Mkoa wa Mtwara litaisha?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Pamoja na majibu hayo ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba mitambo ni michakavu na ni kweli ni ya muda mrefu; je, imejipangaje kununua mitambo mipya ulizingatia kuna ongezeko kubwa la mahitaji ya umeme katika mikoa hiyo ya Lindi na Mtwara?
Swali la pili; ni lini Serikali itaunganisha mfumo wa gesi asilia ili uweze kutumika katika majumba ya Mkoa wa Lindi na Mtwara ukizingatia kwamba kule ndiko gesi inakozalishwa? Nakushukuru.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Tunza Malapo kwa kufuatilia masuala ya umeme katika Mkoa wa Mtwara. Kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya swali la msingi; kwanza, Serikali baada ya kuona uchakavu wa mitambo hii tisa ya Kituo cha Mtwara, imenunua mitambo miwili mipya. Hivi ninavyozungumza, kazi ya ufungaji wa mitambo hii inaendelea ambayo itazalisha megawati nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua Mikoa ya Mtwara na Lindi mahitaji yanaongezeka, Serikali imekuja na mpango wa kujenga mitambo mingine ya kuzalisha umeme megawati 300 kwa kutumia gesi na mpaka sasa Kampuni ya JICA imeendelea na upembuzi yakinifu. Kama ambavyo tumesema kwenye bajeti yetu mradi huu utaanza kutekelezwa mwaka 2018/2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimtoe wasi wasi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeliona hilo na kwamba mradi huu mkubwa wa megawati 300 utatatua matatizo yote katika Mikoa hiyo ya Kusini na pia itaupeleka umeme katika Gridi ya Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameeleza ni lini mpango wa kusambaza…
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Tunza ameulizia ni lini mpango wa kusambaza gesi asilia majumbani katika Mkoa wa Mtwara utaanza? Napenda nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kama ambavyo ameona hivi karibuni tumezindua mpango wa kusambaza gesi asilia katika Mkoa wa Dar es Salaam, lakini Mkoa wa Dar es Salaam unakwenda sambamba na Mikoa ya Mtwara na Lindi. Kwa hiyo, hii kazi itafanyika katika mwaka 2018/2019, tutasambaza gesi katika maeneo mbalimbali kwa matumizi ya majumbani kwa Mikoa hiyo. Ahsante.

Name

John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni lini tatizo la kukatika mara kwa mara kwa umeme katika Mkoa wa Mtwara litaisha?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la kukatika katika kwa umeme liko vilevile kwenye Jimbo la Kibamba kwenye Kata za Kibamba, Kwembe, Msigani, Mbezi, Saranga na Goba ambako kuna tatizo vilevile la kupungua kwa umeme (low voltage). Sasa ni hatua gani ambazo Serikali inachukua kuhakikisha kwamba hili tatizo la kukatika katika na kupungua kwa umeme linamalizika?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mnyika juu ya suala la kukatika katika kwa umeme kwa maeneo ya Jimbo lake la Kibamba pamoja na Kata alizozitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtaarifu Mheshimiwa Mnyika, Serikali kupitia Shirika la TANESCO lina mpango wa kujenga kituo kikubwa cha kupokea na kupoozea umeme maeneo ya Kibamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo anafahamu katika Mkoa wa Dar es Salaam kulikuwa na ukarabati wa miundombinu ya umeme na ujenzi wa vituo mbalimbali hasa baada ya kuongezeka kwa mahitaji; na ilionekana ile njia ya msongo wa KV132 inayotoka Ubungo kupeleka umeme katika maeneo mbalimbali imezidiwa, hivyo baada ya kukamilika kwa vituo vya Gongo la Mboto, Kipawa, Mbagala na Kurasini, Serikali sasa kupitia TANESCO imejielekeza katika ujenzi wa kituo hicho cha Kibamba.
Kwa hiyo, naomba niendelee kuwahimiza watu wa TANESCO wafanye haraka huo mradi uanze ili uweze kutatua matatizo ya kukatika katika kwa umeme na low voltage katika Jimbo la Kibamba na Kata alizozitaja. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni lini tatizo la kukatika mara kwa mara kwa umeme katika Mkoa wa Mtwara litaisha?

Supplementary Question 3

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Tatizo la kukatika kwa umeme katika Mji wa Mtwara limefanana kabisa na Moshi Manispaa. Moshi umeme huwa unakatika sana na hata ukirudi, unarudi mdogo sana.
Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha Moshi inapata umeme wa uhakika ukizingatia Moshi ni Mji wa viwanda?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge Lucy Owenya wa Viti Maalum swali lake kuhusu kukatika katika kwa umeme kwa maeneo ya Moshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme wakati mwingine sababu zinazopelekea kukatika kwa umeme ni uchakavu wa miundombinu ya kusafirishia umeme. Kwa kuliona hilo, Serikali kupitia ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, umekuja na mradi wa ujenzi wa njia ya Msongo wa KV 400 unaotoka Singida mpaka Namanga ambao huo pia utatumika kusafirishia umeme ambao utakuwa wa kutosha kufika maeneo ya Moshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, tuna ujenzi pia wa njia ya msongo wa KV 400 ambao utatoka Kinyerezi – Kibaha – Chalinze – Segera na Moshi. Kwa hiyo, nataka nimthibitishe Mheshimiwa Mbunge kwamba hilo suala limeonekana kwa kuwa mahitaji ya umeme kwa ajili ya viwanda yameongezeka sana Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, ndiyo maana Serikali inataka kutekeleza hiyo miradi ili umeme unaozalishwa kwa wingi usafirishwe na uweze kutumika. Ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni lini tatizo la kukatika mara kwa mara kwa umeme katika Mkoa wa Mtwara litaisha?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Tatizo lililopo Mtwara linafanana kabisa na tatizo lililopo Mkoa wa Kagera. Umeme ukatika mara kwa mara hasa Bukoba Mjini, Bukoba Vijijini, Muleba, Missenyi na Karagwe. Je, ni lini tatizo hili la kukatika umeme litakwisha?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Oliver naye ameuliza ni lini Mkoa wa Kagera suala la kukatika kwa umeme litapungua kama siyo kumalizika kabisa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli tunatambua Mkoa wa Kagera ambao kwanza wanapata umeme kutokea Uganda, tunanunua kama megawati 10 kutoka Uganda ambazo tunazisambaza katika maeneo yale, lakini Serikali pia kwa kuliona hilo, ndiyo maana sasa imejitahidi kuunganisha Wilaya za Ngara na Biharamulo kwenye Gridi ya Taifa. Mkakati huo unaendelea na pia tuna mpango wa kujenga transmission line ili umeme ambao utazalishwa katika maeneo ya Rusumo ambao tumeingiza megawati 80 tuweze kusambaza katika maeneo ya Mkoa wa Kagera na kuweza kutatua tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namshukuru Mheshimiwa Mbunge na ninampongeza kwa ufuatiaji wake na Wabunge wote wa Viti Maalum ambao wanafuatilia sekta ya nishati, nawashukuru sana.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni lini tatizo la kukatika mara kwa mara kwa umeme katika Mkoa wa Mtwara litaisha?

Supplementary Question 5

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa tatizo lililopo katika Mkoa wa Mtwara linafanana na kukatika kwa umeme katika eneo la Kigogo Mkoani Dar es Salaam tena bila taarifa; je, Serikali ina mkakati gani wa kukabiliana na kadhia hii? Ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mheshimiwa Toufiq amekuwa akifuatilia mara kwa mara suala hili la kukatika kwa umeme kwa maeneo ya Kigogo. Kupitia mpango wa Serikali na Shirika lake la TANESCO, tunajenga sub-station maeneo ya Mburahati ambapo sub-station hiyo itasaidia kumaliza kabisa tatizo la kukatika kwa umeme maeneo ya Kigogo. Nakushukuru.

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni lini tatizo la kukatika mara kwa mara kwa umeme katika Mkoa wa Mtwara litaisha?

Supplementary Question 6

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo la kukatika kwa umeme Mkoani Mtwara linafanana sana na tatizo la kukatika kwa umeme katika Kisiwa cha Mafia. Kisiwa cha Mafia kinapata umeme kutoka kwenye majenereta manne makubwa ya dizeli. Kwa kuwa Mheshimiwa naibu Waziri amesema Mkoa wa Mtwara una majenereta 11 yakiwemo mawili mapya; je, haoni sasa ni muhimu tuchukue yale majenereta mawili mapya ya Mtwara na kuyapeleka mafia?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa shahidi, Mheshimiwa Mbaraka Dau ameshauliza maswali zaidi ya mawili kwa tatizo la umeme la Mafia. Naomba nimthibitishie kwamba Serikali kama ambavyo imepata kumjibu ndani ya Bunge, tunalishughulikia kwa karibu tatizo la upatikanaji wa umeme katika Wilaya ya Mafia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hilo swali alilosema kwamba tupeleke mashine mbili, naomba nimwombe kaka yangu, nami pia ni Mbunge wa maeneo hayo kwamba hili suala aje Ofisini tulizungumze, lakini kwa sasa zile mashine lazima zitumike Mtwara na Mafia tutafanya utaratibu mwingine. Ahsante sana.