Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 45 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 384 2018-06-06

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:-
Je, ni lini tatizo la kukatika mara kwa mara kwa umeme katika Mkoa wa Mtwara litaisha?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara katika Mikoa ya Mtwara na Lindi inayopata umeme katika kituo cha kuzalisha umeme kutumia gesi asilia kilichopo Mkoani Mtwara kulitokana na kuharibika kwa mitambo ya kuzalishai umeme iliyochangiwa na uchakavu wa mitambo hiyo pamoja na urefu wa miundombinu ya kusambaza umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) imechukua hatua mbalimbali ili kutatua tatizo la kukatika kwa umeme katika mikoa hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua hizo ni pamoja na kutekeleza mradi wa ujenzi wa vituo viwili vya kukuza na kupoza umeme vyenye uwezo wa 132/33KV na 20MVA vilivyopo Mtwara Mjini na Mahumbika Mkoani Lindi, pamoja na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolt 132 ya umbali wa kilomita 80 kutoka Mtwara hadi Mahumbika. Mradi huu umekamilika na umeanza kufanya kazi rasmi mwezi Mei, 2018 na gharama ya mradi ni shilingi bilioni 16.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANESCO imekamilisha ukarabati wa mitambo minane na mtambo mmoja uliosalia, Mzabuni wa Kampuni ya MANTRAC anaendelea na kazi ya kukarabati na inatarajia kukamilika mwezi Juni, 2018. Ili kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya umeme katika Mikoa ya Mtwara na Lindi, TANESCO imenunua generator mbili zenye uwezo wa kufua umeme wa megawatts 4 na kazi ya kufunga mitambo hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua nyingine Mikoa ya Lindi na Mtwara imeunganishwa na Gridi ya Taifa kupitia njia ya umeme ya kilovolti 33 ambapo Mikoa hiyo sasa inapata umeme kutoka kituo cha kuppoza umeme cha Mbagala na hatua hii imeimarisha hali ya upatikanaji wa umeme na hivyo kukipunguzia mzigo kituo cha kuzalisha umeme cha Mtwara.