Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya mpya ya Buhigwe na kutoa vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi?

Supplementary Question 1

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nashukuru majibu ya Serikali. Ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, tunacho Kituo cha Mlyama ambacho kimejengwa kwa muda mrefu sasa hakijamalizika na Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani analijua hilo na pale Wilayani tuna kituo ambacho kinatumiwa kwenye nyumba ambayo siyo nzuri na haitoshi; na kwa majibu haya kwamba wametenga eneo; swali linauliza kwamba ni lini wanaanza kujenga? Hayo maeneo tunashukuru wanayo, lakini swali, wanaanza kujenga lini?
Mheshimiwa Spika, la pili; tuna matukio makubwa sana ya ujambazi yanayotokea hasa baada ya Wakimbizi kurudishwa kwenda Burundi na Jimbo langu linavamiwa kila siku iendayo kwa Mungu na juzi mwanajeshi mmoja ameuawa baada ya kuwa wameenda ku-intervene mashambulio hayo na vitendea kazi ni hafifu.
Je, ni lini sasa vitendea kazi vya magari na pikipiki vitaongezwa kwenye Wilaya ile? Yeye mwenyewe anayo taarifa kwamba ujambazi ni kila siku. Nakushukuru.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na lini kituo hiki kitajengwa; nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kutambua changamoto ya location ya Jimbo lake, pale ambapo tutapata fedha ni katika vituo ambavyo tutavipa kipaumbele.
Mheshimiwa Spika, sambamba na kujibu swali lake la pili ambalo litahusisha vilevile pamoja na upelekaji wa vitendea kazi ili tuweze kukabiliana na changamoto ambayo ameizungumza ambayo tunaitambua na tumeshaanza kushughulika nayo.

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya mpya ya Buhigwe na kutoa vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi?

Supplementary Question 2

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Katika Kata za Jiji la Tanga miaka ya 1990, kata zilihamasishwa kujenga vituo mbalimbali vya Polisi ambavyo vilisaidia kupunguza uhalifu, matokeo yake sasa hivi vituo vile vimetelekezwa, vimekuwa ni nyumba za vibaka.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kuvifufua vituo hivyo ili kuweza kuweza kuzuia uhalifu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, mara zote tumekuwa tukihamaisha Waheshimiwa Wabunge na wananchi kushirikiana na Serikali katika kukabiliana na upungufu wa Vituo vya Polisi nchini. Kwa hiyo, ni jambo la ajabu sana kama Serikali tutakubali kuona kwamba jitihada hizi za wananchi wanavunjwa moyo.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba siyo dhamira ya Serikali kuvitelekeza vituo hivyo ambavyo vina umuhimu mkubwa.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu Mheshimiwa Mbunge hakutaja kituo gani ambacho kimetelekezwa, kwa hiyo, ni vigumu kumpa sababu ya kituo hicho ambacho amekusudia kwamba hakitumiki mpaka sasa hivi kwa sababu gani? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, baada ya Bunge hili nitakuwa tayari kukutana naye ili aweze kunipa taarifa za kina tufuatilie na kuchukua hatua za haraka. (Makofi)