Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 105 2018-09-13

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya mpya ya Buhigwe na kutoa vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Albert Obama Ntabaliba, Mbunge wa Buhigwe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto za miundombinu Kijiografia pamoja na nyinginezo zinazoikabili pamoja na mikoa mipya hapa nchini. Changamoto hizi ni pamoja na uhaba wa Ofisi na nyumba za kuishi watumishi. Hata hivyo, Jeshi la Polisi katika Wilaya mpya ya Buhigwe limeshatenga eneo kwa ajili ya Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya na Kituo cha Polisi cha Wilaya chenye ukubwa wa ekari tano. Pia zimetengwa ekari 20 kwa ajili ya nyumba za makazi ya Askari Polisi. Aidha, kwa sasa huduma za kipolisi katika maeneo ya Buhigwe hutolewa kupitia kituo kidogo cha Polisi cha Buhigwe na Manyovu.
Mheshimiwa Spika, mahitaji ya vituo vya polisi pamoja na nyumba za makazi ya askari nchini ni makubwa na yanahitaji fedha nyingi. Haya hivyo, Jeshi la Polisi limeweka vipaumbele katika Mikoa na Wilaya mpya, Miji inayokuwa kwa kasi pamoja na maeneo yenye viashiria na matishio ya kiusalama ili kutoa huduma bora kwa wananchi.