Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Wilaya ya Itilima haina Kituo cha Polisi cha Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Itilima?

Supplementary Question 1

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; Wilaya ya Itilima Makao Makuu yake yako Kata ya Lagangabiliri na Kituo cha Polisi kipo Kata ya Luguru. Je, Serikali ina mpango gani kuhamishia Kituo cha Polisi katika Makao Makuu ya Wilaya ya Itilima? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kituo kinachotumika kwa sasa kilitolewa kwa hisani ya Ndugu Paulo Ng’hwani kwa muda mrefu na kituo hicho kwa maana ya hilo jengo limeharibika, je, mna mkakati gani sasa wa kupeleka fedha angalau kukarabati jengo hilo ambalo lilitolewa kwa hisani ya Ndugu Paulo Ng’hwani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kwanza kutoa pongezi zangu za dhati kwa Mbunge wa Itilima, Mheshimiwa Njalu ambaye wakati wa ziara yangu nilipofanya kule niliona jitihada zake kubwa sana ambazo amekuwa akizitoa katika kufanikisha kutatua changamoto kwenye eneo la Polisi kwa ujumla wake. Moja kati ya jitihada hizo ni kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa Kituo cha Polisi ambacho sasa hivi kinaendelea na ujenzi wake. Vile vile Mheshimiwa Mbunge aliniahidi kwamba kazi hiyo ataendelea nayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge Dotto naye namshukuru vilevile kwa kuona changamnoto hizo. Naomba tu aendelee kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo na Serikali kwa pamoja tutashirikiana kufanikisha ujenzi ukamilike kwa haraka ili kituo hiki kiweze kutumika. Ukarabati wa kituo kingine utategemea na hali ya upatikanaji wa fedha.