Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 25 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 215 2018-05-09

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:-
Wilaya ya Itilima haina Kituo cha Polisi cha Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Itilima?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Gimbi Dotto Masaba, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi lina jumla ya Wilaya za Kipolisi 168 nchi nzima ambapo kati ya hizo, Wilaya 127 zina majengo kwa ajili ya Ofisi na Vituo vya Polisi vya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, uhaba wa vituo vya polisi pamoja na nyumba za kuishi askari nchini umesababishwa na kukosekana kwa rasilimali za kutosha kukidhi mahitaji ambayo ni makubwa. Hata hivyo, Serikali kupitia Jeshi la Polisi linafanya jitihada mbalimbali kama vile kutumia rasilimali zilizopo katika eneo husika pamoja na kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa vituo vya polisi nchini. (Makofi)