Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. MHE. KEMIREMBE J. LWOTA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha umeme wa uhakika kwenye Kata za Wilaya ya Nyamagana, Mkoa wa Mwanza?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru naomba niulize maswli mawili madogo ya nyongeza na moja ni kwa sababu Serikali bado yako maeneo kwenye Jiji la Mwanza na hasa Wilaya ya Nyamagana kama Kata za Kishiri, Lwanima na Buhongwa bado hayajapata umeme wa uhakika.
Ni lini sasa Serikali kupitia Shirika la TANESCO itahakikisha maeneo hayo yanapata umeme wa kutosha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili Mji wa Mwanza bado unayo maeneo yenye taswira ya vijiji ikiwemo Jimbo la Ilemela. Ni nini mpango wa Serikali kupitisha umeme kwenye maeneo hayo hasa maeneo ambayo tayari yamebaki sambamba na Kata za Sangabuye, Bugogwa, Kahama na Shibula ili kuhakisha Mwanza yote inapata umeme wa uhakika? Ninakushukuru sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ya swali la msingi, nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri. Pia nimpongeze sana Mheshimiwa Mabula pia katika kufuatilia maeneo ya vijiji hivi 18.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa tulitenga fedha shilingi bilioni 8.7 kwa ajili ya kupeleka vijji tisa katika jimbo la Mheshimiwa Mbunge vipya, kupitia mradi wa TANESCO. Na nimwambie tu Mheshimiwa Mabula nimpongeze sana hivi sasa TANESCO wanapeleka umeme katika kijiji cha Lwanima na wakimaliza Lwanima wanakwenda Kanema, pamoja na Bukaga, Nyakwagwe watapeleka. Pia watapeleka mpaka Kigogo pamoja Isebanda na wakimaliza Isebanda Mheshimiwa wanakwenda pia kwenye kijiji cha Kigodo pamoja Nyangwi pamoja na mtaa wako wa Kagera.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimpe uhakika Mheshimiwa Mabula kwamba hadi kufika mwezi Juni ambapo mradi unakamilika wananchi wote wa vijiji vyote vinane, umbali wa kilometa 9.2 utakuwa umefikishiwa umeme na Mwanza itakuwa inapata umeme wa uhakikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swala lake la pili, ni kweli yako maeneo ambayo yako mjini na visiwani na vijiji. Tuna mradi wa (Peri-urban) ambao Jiji la Mwanza katika maeneo ya Kishiri, Buhongwa Pamoja na Kata za Lwanima pia ziko kwenye mpango huo. Kwa hiyo, watapelekewa kupitia mradi wa (Peri-urban) lakini pamoja na mradi wa Densification utakaoanza Julai mwaka huu.