Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y. MHE. ALI HAFIDH TAHIR) aliuliza:- Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa hususan Mawaziri Wakuu Wastaafu ambao wameaminiwa na kuchaguliwa na wanachama wa chama fulani lakini baada ya kupata madaraka wakahama vyama hivyo na kwenda kunufaisha vyama vingine:- Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati sasa wa kuifanyia marekebisho sheria husika ili kufuta stahiki za Mawaziri Wakuu Wastaafu wanaohama vyama vyao kwa kuwa stahiki hizo zilitokana na nguvu za chama alichohama, na kwamba kuendelea kumpa stahiki hizo ni sawa na kuwakejeli na kuwadharau wananchi waliomchagua?

Supplementary Question 1

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, majibu ya Serikali ni sahihi yanaendana na lengo la 16 la Malengo Endelevu ya Dunia ya leo. Kwa kuwa Wabunge majukumu yao ni kuwa na uelewa mkubwa na ni sehemu ya viongozi katika jamii, Waziri haoni umuhimu wa kutoa semina kwa Waheshimiwa Wabunge ambapo watapata uelewa wa kutumia muda wao itakiwavyo kwa maslahi ya Taifa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pili, kwa kuwa Serikali imelitambua hili na inaonekana Waheshimwia Wabunge hawaijui vizuri hata Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na kwa kuwa zipo sheria vile vile zinazoambatana na Katiba ambapo Wabunge tukipata uelewa na hasa majukumu manne ya Mbunge; la kwanza likiwa kwa Taifa lake; la pili, kwa Jimbo lake la uchaguzi; la tatu, kwa chake cha siasa; na la nne, kwa dhamira yake binafsi ili tuweze kupata uelewa wa hali ya juu namna hiyo na Bunge liweze kujenga maslahi kwa Taifa?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kujibu swali moja kama ambavyo umeeleza, ingawa yeye ameweka kama maswali mawili lakini naomba nijikite kwenye swali moja.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na umuhimu wa kutoa semina kwa masuala mbalimbali ya namna ya kutumia muda kuweza kuuliza maswali kama haya, Mheshimiwa Mbunge anayo fursa na anayo haki ya kuweza kuuliza swali lolote. Ndiyo maana sisi kama Serikali tunaona ni fursa muhimu kuweza kutumia Bunge lako Tukufu kujibu maswali kama haya kuweka kuelimisha. Siyo Bunge tu, lakini vile vile Umma mzima wa Tanzania.
Mheshimiwa Spika, suala la namna ya kuelimisha kuhusiana na uelewa wa Katiba, ni jukumu la kila Mheshimiwa Mbunge lakini vile vile na wananchi wote kwa ujumla kuweza kuhakikisha kwamba wanayo elimu ya masuala mbalimbali ya siasa na elimu ya uraia ikiwemo uelewa wa Katiba.

Name

Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y. MHE. ALI HAFIDH TAHIR) aliuliza:- Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa hususan Mawaziri Wakuu Wastaafu ambao wameaminiwa na kuchaguliwa na wanachama wa chama fulani lakini baada ya kupata madaraka wakahama vyama hivyo na kwenda kunufaisha vyama vingine:- Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati sasa wa kuifanyia marekebisho sheria husika ili kufuta stahiki za Mawaziri Wakuu Wastaafu wanaohama vyama vyao kwa kuwa stahiki hizo zilitokana na nguvu za chama alichohama, na kwamba kuendelea kumpa stahiki hizo ni sawa na kuwakejeli na kuwadharau wananchi waliomchagua?

Supplementary Question 2

MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri sana ya Serikali.
Mheshimiwa Spika, hili tatizo siyo la Mheshimiwa Mbunge aliyeuliza peke yake, ni tatizo la nchi nzima, kwamba kumekuwa na tatizo kubwa la kushindwa Sasa swali kwa Mheshimiwa Waziri; ili tuweza kujenga Taifa moja lenye kuheshimu kwamba vyama vingi vya siasa ni takwa la kikatiba kwa mujibu wa Ibara Na. 3 (1) na (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwamba nchi yetu ni ya vyama vingi vya siasa; hatuoni kama kuna sababu za msingi za Serikali kukemea watumishi wa Serikali ambao wanafikiri wana haki ya kutenda haki kwa chama kinachotawala lakini kutokutenda haki kwa vyama vingine ambavyo ni tofauti na Chama cha Mapinduzi? (Makofi)kutofautisha majukumu ya Chama cha Mapinduzi na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tatizo la baadhi ya watumishi katika Serikali kufikiria wao ni sehemu ya Chama Tawala, limekuwa ni tatizo kubwa ambalo linapekea kutokutenda haki katika maeneo mengi sana ya Taifa letu. Swali la Mheshimiwa Mbunge siyo kwamba linajenga tu misingi ya kibaguzi, linajenga misingi ya kichochezi kwamba nihaini kuwa kwenye chama kingine tofauti na Chama cha Mapinduzi; na jambo hili liko katika ngazi mbalimbali za utawala katika nchi yetu. (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Spika, kwanza niseme tu kwamba swali hili sisi binafsi kwa upande wa Serikali hatujaliona kama ni la uchochezi na ndiyo maana tumeweza kulijibu na ninaamini upande wa pili wameweza kufurahia majibu ambayo tumeyajibu kwa sababu tumetenda haki kwa mujibu wa Katiba. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kwamba watumishi wengine wamekua labda hawatendi haki kwa vyama vingine, kwa kweli sidhani kama ni sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Watumishi wa Umma wanatakiwa watekeleze sera za Serikali; wanatambua kwamba kuna Mfumo wa Vyama vingi vya Siasa, lakini vilevile wanatambua kwamba ipo Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ambacho ndicho Chama kinatawala katika wakati husika. Kwa hiyo, hawana jinsi, wanatumikia kwa kufuata Ilani ya chama kilichopo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ukiangalia kwa wao, pamoja na kwamba wanatumikia chama kilichopo madarakani, yapo makatazo. Hawatakiwi kujionyesha dhahiri kwamba wanahusika katika masuala ya kisiasa. Ndiyo maana ukiangalia katika sehemu (f) ya Kanuni zetu za Kudumu za Utumishi wa Umma za mwaka 2009 imeeleza ni kada gani ambazo hazitakiwi kujihusisha na masuala ya kisiasa. Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y. MHE. ALI HAFIDH TAHIR) aliuliza:- Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa hususan Mawaziri Wakuu Wastaafu ambao wameaminiwa na kuchaguliwa na wanachama wa chama fulani lakini baada ya kupata madaraka wakahama vyama hivyo na kwenda kunufaisha vyama vingine:- Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati sasa wa kuifanyia marekebisho sheria husika ili kufuta stahiki za Mawaziri Wakuu Wastaafu wanaohama vyama vyao kwa kuwa stahiki hizo zilitokana na nguvu za chama alichohama, na kwamba kuendelea kumpa stahiki hizo ni sawa na kuwakejeli na kuwadharau wananchi waliomchagua?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, kwa kawaida viongozi wa kisiasa hawapati pensheni bali sisi kama Wabunge tunapata gratuity. Isipokuwa viongozi wetu hawa wakuu ambao muuliza swali amewazungumzia kwamba wao wanapewa pensheni wakiamini kwamba wameshamaliza kazi na wanatulia na wanapewa pensheni ili wasitapetape na kuhangaika kwenda hapa na pale kuhemea.
Je, huoni sasa ni wakati wa kuirekebisha sheria kwamba pensheni hiyo itolewe pale tu ambapo tumeshajiaminisha kwamba kiongozi huyu sasa ameshastaafu kweli, anastahili pensheni na kwamba hatatapatapa tena mpaka kufikia hatua ya kukataa kwamba hajafanya kazi yoyote? (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Spika, ukiangalia stahili mbalimbali ikiwemo na pensheni au pensheni ya mwaka, iko kwa mujibu wa sheria; Sheria Na. 3 ya mwaka 1999 lakini vilevile iko kwa mujibu wa marekebisho ya Sheria Na.11 ya mwaka 2005.
Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza, bado mtu anayo haki. Nami nitoe tu rai kwamba kwa wale Viongozi Wakuu Wastaafu ambao wanahudumiwa kwa mujibu wa sheria hii ambayo niliitaja ya mwaka 1999 pamoja na mwaka 2005, wajitahidi kuenenda na misingi ya Kifungu Na. 6(j) aya ya tatu, imeweka masharti kwa Viongozi wa Umma, ni masuala gani wanatakiwa wayafuate.
Mheshimiwa Spika, hawatakiwi kutoa siri za Serikali walizozipata wakati wakitumikia; hawatakiwi kutoa masuala mbalimbali ambayo waliyapata wakati wakitumikia kama viongozi wa umma; hawakatazwi kujiunga na masuala mengine kwa sababu Sheria haijakataza.
Mheshimiwa Spika, mimi naomba kwa wale viongozi wa umma wa kisiasa, basi wajikite katika misingi ya kifungu Na. 6(j)(3) cha Sheria ya Maadili; Sheria Na. 13 ya mwaka 1995. (Makofi)

Name

Hafidh Ali Tahir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y. MHE. ALI HAFIDH TAHIR) aliuliza:- Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa hususan Mawaziri Wakuu Wastaafu ambao wameaminiwa na kuchaguliwa na wanachama wa chama fulani lakini baada ya kupata madaraka wakahama vyama hivyo na kwenda kunufaisha vyama vingine:- Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati sasa wa kuifanyia marekebisho sheria husika ili kufuta stahiki za Mawaziri Wakuu Wastaafu wanaohama vyama vyao kwa kuwa stahiki hizo zilitokana na nguvu za chama alichohama, na kwamba kuendelea kumpa stahiki hizo ni sawa na kuwakejeli na kuwadharau wananchi waliomchagua?

Supplementary Question 4

MHE. ALI HAFIDH TAHIR: Mheshimiwa Spika, kwanza nakushukuru kwa kuniona na ninawashukuru wale wote ambao walinisaidia katika kuuliza maswali ya ngongeza.
Mheshimiwa Spika, la kwanza nataka niweke indhari kwamba wale watumishi wa Serikali ambao tuliambiwa labda hawataweza kuingia katika mambo ya siasa, humu ndani ya Bunge hivi sasa kuna mwenzetu mmoja alishawahi kuwa Katibu Mkuu; na hivi sasa yumo ndani ya Bunge hili kwa upande upinzani. Hilo la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, la pili, nilichokuwa nazungumzia katika swali langu ni ulafi wa madaraka. Ndicho nilichokuwa nazungumza! Nimesema mtu anapomaliza Uwaziri Mkuu kwa kupitia Chama cha Mapinduzi au chama kingine chochote, iweje tena aitumie nafasi ile ambayo aliipata katika Chama cha Mapinduzi kwenda katika chama kingine kudai nafasi ya uongozi? Hicho ndicho nilichokuwa nakiulizia. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, mifano miwili hai hivi sasa, tuna Mawaziri… (Kelele)
MHE. ALI HAFIDH TAHIR: Mheshimiwa Spika, kuna Mawaziri Wakuu wawili ambao hivi sasa, mmoja kati ya hao ameshawahi kugombea urais akakosa; swali langu liko pale pale, pensheni hizi zinakwendaje? Kwa mfano, angeshinda Urais ingekuaje? Ndiyo swali langu kubwa muhimu hilo. Ulafi wa madaraka! (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali la kwanza kwenye makatazo, tunatoa elimu kwa umma. Hayanipi taabu!
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali la kwanza kwenye makatazo ya viongozi wa utumishi umma ambao wamekua wakikatazwa kugombea nafasi za siasa na ametolewa mfano wa Mbunge, Mheshimiwa Ruth Mollel, ambaye alikuwa ni Katibu Mkuu katika Wizara mbalimbali; kwa faida ya hadhira hii, ukiangalia katika sehemu (f) kama nilivyoeleza mwanzoni ya kanuni za kudumu, inaeleza kwamba watumishi walioajiriwa katika Taasisi zifuatazo; Jeshi la Wananchi na Jeshi la Kujenga Taifa, Usalama wa Taifa…
MHE. ANGELLAH JASMINE KAIRUKI - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Nimepewa nafasi, naomba tupeane fursa.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa watumishi ambao wanakatazwa kujiunga au kushiriki katika masuala ya kisiasa ni watumishi walioko katika Jeshi la Wananchi na Jeshi la Kujenga Taifa, watumishi walioko katika Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza, Uhamiaji, Jeshi la Zimamoto, Mgambo, TAKUKURU, Ofisi ya Bunge, Msajili wa Vyama vya Siasa, Mawakili wa Serikali, Majaji na Mahakimu.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Katibu Mkuu huyu kama ambavyo nimeeleza, itaonekana ni dhahiri kwamba hajawekewa katazo.
Mheshimiwa Spika, katika swali la pili, alitaka kujua iweje sasa Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Lowassa aweze kutumia tena nafasi hii kuomba nafasi nyingine? Kama nilivyoeleza kupitia Ibara ya 20, haijaweka katazo, kwa hiyo, unaona ni dhahiri anayo haki hiyo. Pia alitaka kujua endapo angeshinda Urais ingekuaje? Mimi nadhani tungevuka daraja wakati huo tumelifikia. (Makofi)