Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 2 Good Governance Ofisi ya Rais TAMISEMI. 18 2016-01-27

Name

Hafidh Ali Tahir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. JAMES F. MBATIA (K.n.y. MHE. ALI HAFIDH TAHIR) aliuliza:-
Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanasiasa hususan Mawaziri Wakuu Wastaafu ambao wameaminiwa na kuchaguliwa na wanachama wa chama fulani lakini baada ya kupata madaraka wakahama vyama hivyo na kwenda kunufaisha vyama vingine:-
Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati sasa wa kuifanyia marekebisho sheria husika ili kufuta stahiki za Mawaziri Wakuu Wastaafu wanaohama vyama vyao kwa kuwa stahiki hizo zilitokana na nguvu za chama alichohama, na kwamba kuendelea kumpa stahiki hizo ni sawa na kuwakejeli na kuwadharau wananchi waliomchagua?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI - WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hafidh Ali. Tahir, Mbuge wa Dimani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mawaziri Wakuu Wastaafu wanahudumiwa kwa mujibu wa Sheria ya Mafao kwa hitimisho la kazi kwa viongozi, Sheria Na. 3 ya mwaka 1999. Sheria haielezi hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa Waziri Mkuu Mstaafu atakayeamua kuhamia chama kingine cha Siasa tofauti na chama kilichomweka madarakani na kumwezesha kushika wadhifa wa Waziri Mkuu.
Mheshimwa Spika, mbali na sheria hiyo kutoweka zuio lolote kwa Viongozi wa Kifaifa Wastaafu kujiunga na chama kingine cha siasa, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inalinda haki za msingi za binadamu ikiwemo haki ya uhuru wa mtu kujihusisha na masuala ya Siasa. (Makofi)
Kwa mujibu wa Ibara ya 20(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatamka kwamba mtu yeyote anayo haki ya kujihusisha na mambo ya kisiasa na kuweza kujiunga na chama chochote. Mawaziri Wakuu Wastaafu kama walivyo watu wengine, wanao uhuru wa kujiunga na chama chochote cha kisiasa wanachopenda ili mradi hawavunji sheria.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa haki ya kujiunga na chama chochote au kujihusisha na masuala ya kisiasa ni haki ya Kikatiba, na kwa kuwa haki hizi haziwezi kuzuiwa au kuingiliwa, ni wazi kwamba suala la kufanyia marekebisho Sheria ya Mafao kwa Viongozi wa Kitaifa Wastaafu, Sheria Na. 3 ya mwaka 1999 kwa lengo la kuwazuia Mawaziri Wakuu Wastaafu au Viongozi wengine wa Kitaifa Wastaafu kujiunga na chama chochote cha kisiasa itakuwa ni kwenda kinyume na Katiba ya nchi. (Makofi)