Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kituo cha Polisi Bububu ni kikongwe sana na pia kimechakaa sana na kinahitaji ukarabati mkubwa. Je, ni lini kituo hicho kitafanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini kidogo hayaniridhishi, kwa sababu yeye mwenyewe Naibu Waziri amekwenda kujionea kituo hicho cha Bububu, alikitembelea.
Je, kituo kile kwa sababu hakina computer, hakina photocopy machine na mpaka hivi sasa hivi wanaenda kutoa photocopy nje ya kituo. Ni lini Serikali itachukua hatua ya kukipatia computer na photocopy machine?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa sababu huko nyuma niliulizwa suala la gari ya polisi, kwa sababu kituo changu kipo barabarani na kina uhalifu mwingi katika Jimbo langu la Bububu.
Je, ni lini Serikali itatupatia gari hilo la Polisi ili kupunguzia wananchi usumbufu? Kwa sababu sasa hivi wakiomba gari binafsi wanachukua ili kwenda kusaidia kufanya doria?
Naiomba Serikali ijitahidi ili kituo changu kipate gari ya doria ili kupunguza usumbufu kwa wananchi. Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mwantakaje kwa jitihada zake za kuhakikisha kwamba mazingira ya askari wetu hasa katika Kituo cha Polisi Bububu katika Jimbo lake yanakuwa mazuri.
Mheshimiwa Spika, ni kweli tulifanya ziara ya pamoja kwenye kituo hiki na kuna mambo mengi tuliyarekebisha, lakini nimhakikishie, kama tumeweza kurekebisha mambo makubwa ambayo mwenyewe anafahamu, sidhani kama hili la photocopy na computer litatushinda. Nimwombe tu avute subira, tutalifanyia kazi.
Mheshimiwa Spika, upande wa suala la pili kuhusiana na gari, kwa sasa bado hatuna magari, lakini tunatarajia kupata magari. Kwa hiyo, tutaangalia ukubwa wa changamoto zilizopo nchi nzima, kwa sababu upungufu haupo Bububu peke yake, yako maeneo mbalimbali nchini. Kwa hiyo, kadri ya idadi ya magari itakapopatikana, tutaangalia uwezekano vilevile wa kukipatia Kituo cha Polisi cha Bububu. (Makofi)

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kituo cha Polisi Bububu ni kikongwe sana na pia kimechakaa sana na kinahitaji ukarabati mkubwa. Je, ni lini kituo hicho kitafanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 2

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali aliloulizia Mheshimiwa aliyezungumza sasa hivi, halina tofauti kabisa na Gereza la Keko ambalo miundombinu yake ni mibaya na pia kuna msongamano mkubwa sana wa wafungwa na wengi wao zaidi ya nusu ni mahabusu na hivyo hivyo kwenye Gereza la Segerea.
Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba justice inakuwa dispense, mapema watu watoke na magereza yawe na wafungwa ambao ndio wangestahili kukaa pale na hiyo miundombinu iliyokuwepo? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, tunakiri juu ya tatizo la msongamano, kwani ukiangalia takribani Magereza yote kwa ujumla nchini ukiachia mbali la Keko na mengine, mpaka leo tunavyozungumza, tuna takriban wafungwa wanaokadiriwa kufika mpaka 40,000 na wakati capacity ya Magereza yetu haizidi 30,000. Kwa hiyo, utakuta tuna idadi ya wafungwa kama 10,000 hivi ambao wamezidi kiwango magerezani.
Mheshimiwa Spika, kwa kutambua hilo, ndiyo maana Serikali inachukua jitihada mbalimbali kupunguza msongamano huu ikiwemo kupitia zile sheria nne tulizozipitisha hapa Bungeni za kuwapatia kifungo cha nje wafungwa kwa utaratibu wa parole, lakini pia utaratibu wa community services za EML, lakini pia kwa kupitia msamaha wa Rais. Tunampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa jitihada zake alizochukua za kupunguza idadi ya wafungwa mwaka 2017.
Mheshimiwa Spika, pia moja ya jitihada ambazo Serikali inachukua, ni kuhakikisha kwamba tunatenga bajeti ya kutosha kadri ya hali ya fedha inavyoruhusu kupanua Magereza yetu yaweze kuwa na ukubwa zaidi na kuongeza magereza mengine nchini.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hizo ndizo jitihada ambazo tunachukua na tunaamini kabisa kadri tunavyokwenda hivi, sasa hivi uchumi wetu wa nchi, unakwenda vizuri, naamini miaka ya mbele tatizo la msongamano litapungua kama siyo kuisha kabisa.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kituo cha Polisi Bububu ni kikongwe sana na pia kimechakaa sana na kinahitaji ukarabati mkubwa. Je, ni lini kituo hicho kitafanyiwa ukarabati?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona na kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, mwuliza swali alikuwa anauliza kuhusu ukarabati wa kituo, lakini kwa kuwa Wilaya ya Kilolo ni ya siku nyingi sana na haijawahi kujengewa Makao Makuu ya OCD yalipo Makao Makuu ya Wilaya toka imeanzishwa, na kufanya OCD kukaa mbali na DC. (Makofi)
Je, ni lini sasa Serikali itaona umuhimu wa kujenga Makao Makuu ya Polisi yalipo Makao Makuu ya Wilaya ya Kilolo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, ni sahihi kabisa, Kilolo hatuna Kituo cha Polisi cha Wilaya na hii ni moja ya vituo 65 vya wilaya nchini ambavyo hatunavyo na ambavyo vipo katika mpango wa Serikali wa kuvijenga. Kwa hiyo, Kilolo ni kimojawapo.
Mheshimiwa Spika, wakati jitihada hizi za Serikali za kuweza kuona jinsi gani tunafanya kujenga vituo 65 zinaendelea, basi nataka nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanya ziara katika Mkoa wa Iringa hivi karibuni ili tushirikiane tuangalie namna gani nyingine ambayo tunaweza tukafanya ili kuweza kuunga mkono jitihada za Serikali za kujenga kwa kushirikisha wadau mbalimbali.