Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 5 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 39 2018-04-09

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:-
Kituo cha Polisi Bububu ni kikongwe sana na pia kimechakaa sana na kinahitaji ukarabati mkubwa. Je, ni lini kituo hicho kitafanyiwa ukarabati?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, na mimi naomba niungane na Waheshimiwa wengine kumshukuru Mwenyezi Mungu kukujalia kuungana na sisi leo ukiwa mzima. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, Mbunge wa Bububu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua uchakavu wa vituo vya polisi vikongwe nchini kikiwemo Kituo cha Polisi cha Bububu. Jeshi la Polisi lina mpango wa kuvikarabati vituo hivyo kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Aidha, ukarabati wa vituo hivyo vya Polisi kikiwemo Kituo cha Polisi Bububu utafanyika ili kuboresha mazingira ya kazi kwa askari wetu ili kuwawezesha kutoa huduma bora kwa wananchi. (Makofi)