Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESS M. MARWA aliuliza:- Kumekuwa na tatizo kubwa la dawa katika Hospitali ya Manyamanyama iliyoko Wilayani Bunda na hii ni kutokana na hospitali hiyo kutokuwa na hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya:- (a) Je, ni lini Serikali itaipa Hospitali ya Manyamanyama Hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya ili kuongeza mgao wa dawa na kupunguza shida kubwa wanayoipata wananchi? (b) Je, ni lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika hospitali hiyo ili kuongeza ufanisi?

Supplementary Question 1

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Bado sijaridhishwa na majibu hayo ya Mheshimiwa Waziri. Kutokana na sintofahamu ya wananchi hao wa Bunda, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri, nina evidence hapa nisome. Kutokana na kituo hicho cha afya kwa mwaka 2006, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ni Rais Mstaafu aliweka jiwe la msingi. Aliweka jiwe la msingi ili kusudi huo upembuzi yakinifu na hivyo vitu vingine vikikamilika ipewe hati ya kuwa Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kufanya huo upembuzi yakinifu anaousema hapa Mheshimiwa Waziri, mochwari imeshatengenezwa tayari na ipo, chumba cha dharura Mheshimiwa Waziri kipo, X-Ray tayari ipo, Ultra Sound tayari ipo na barua hii nitamkabidhi nikitoka hapa Mheshimiwa Naibu Waziri, ya Wilaya ile lakini pia chumba cha dhararu kipo. Je, ni nini sasa kinachosababisha hii Wilaya ya Bunda na hicho Kituo cha Manyamanyama kisipewe hadhi?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa usimamizi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, Bibi Janet Mayanja akiwa na Madiwani wake chini ya Mwenyekiti wa Halmashauri kutokana na mapato na makusanyo ya Halmashauri wameweza kuweka vitu hivyo na vinginevyo. Ni kwa nini sasa hospitali hiyo isipewe hati? Kama mnatuelezea kwamba vituo vya afya vinatakiwa vibaki palepale ziwepo Hospitali za Wilaya, Mheshimiwa Waziri naomba majibu leo kwamba kama fedha ipo… (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali bado halijakwisha, naomba Mheshimiwa Waziri niambiwe kwamba ni lini sasa na sisi mtatuletea hiyo pesa ya kujenga Hospitali ya Wilaya ili tujue kile ni kituo cha afya? Mheshimiwa Naibu Waziri, tafadhali naomba majibu ya kutosha. Ahsante. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli idadi ya wagonjwa wanaokwenda kupata huduma katika Kituo cha Afya cha Manyamanyama ni wengi sana na ndiyo maana kumekuwa na concern ya kwamba ni vizuri kituo cha afya kile kikapandishwa hadhi ya kutoka kituo cha afya kikawa hospitali ya wilaya. Hata hivyo, ni ukweli usiopingika kwamba uhitaji wa vituo vya afya bado uko pale pale na ujenzi wa hospitali za wilaya bado uko pale pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninachoomba Mheshimiwa Mbunge pamoja na kazi nzuri ambayo anaifanya ya kuhakikisha afya za watu wake zinaimarika, ni vizuri tukahakikisha tunaheshimu ramani inayohusu hospitali ya wilaya ambayo ni tofauti na ramani inayohusu kituo cha afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hospitali za wilaya ambazo tunakwenda kuzijenga kwa mwaka wa 2018/2019, Bunda DC ni miongoni mwa Wilaya ambazo zinakwenda kupata hospitali za wilaya. Kwa taarifa nilizonazo Bunda DC na Bunda Mji, Bunda DC mpaka sasa hivi bado hawajajua wapi Halmashauri yao itakuwa. Kwa hiyo, pesa hiyo ambayo itakuwa ipo tayari kwa ajili ya kujenga hospitali ya wilaya busara itumike ili pale ambapo papo tayari tuanze kujenga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilipata fursa ya kuongea na Mkurugenzi jana, pamoja na Kituo cha Afya cha Manyamanyama tayari Halmashauri imeanza kutafuta eneo lingine la ukubwa wa hekari 40. Kwa hiyo, thinking yao ni kuhakikisha kwamba kunakuwa na eneo mbadala kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya. Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. AGNESS M. MARWA aliuliza:- Kumekuwa na tatizo kubwa la dawa katika Hospitali ya Manyamanyama iliyoko Wilayani Bunda na hii ni kutokana na hospitali hiyo kutokuwa na hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya:- (a) Je, ni lini Serikali itaipa Hospitali ya Manyamanyama Hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya ili kuongeza mgao wa dawa na kupunguza shida kubwa wanayoipata wananchi? (b) Je, ni lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika hospitali hiyo ili kuongeza ufanisi?

Supplementary Question 2

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Katika Bunge lililopita niliuliza swali kuhusiana na hospitali ya wilaya ambayo tulikuwa tumeambiwa kwamba itajengwa katika Kata ya Chipaka kwenye Kijiji cha Chipaka. Sasa hivi inaonesha kwamba kuna mabadiliko ambayo yanataka kufanyika hospitali ile ikajengwe maeneo mengine ambayo hayana majengo kabisa.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo tulilokuwa tumeliteua ni eneo ambalo lilikuwa na majengo ambayo yalikuwa yanatumika kwa ajili ya mradi wa kujenga barabara kutoka Tunduma kwenda Sumbawanga, kuna majengo zaidi ya 20, leo hii wanataka kupeleka maeneo ambayo hayana majengo kabisa. Mheshimiwa Waziri aliniambia hapa atahakikisha kwamba analifuatilia jambo hili na hospitali inajengwa eneo ambalo walikuwa wametuambia kwamba ni lazima itajengwa pale. Je, amefuatilia na anatoa majibu gani kwa wananchi wa Tunduma ili wawe na uhakika wa hospitali katika eneo la Chipaka na Kata ya Chipaka? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali la nyongeza la Mheshimiwa Marwa nimeeleza kwamba ramani kwa ajili ya hospitali za wilaya ambazo zimekuwa designed na Ofisi ya Rais, TAMISEMI zinajitosheleza. Katika pesa ambazo tunakwenda kuanzia tunakwenda kuanza na jumla ya shilingi bilioni 1.5 kwa ramani ambayo ni sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa asingependa tukaenda kwenye majengo ambayo hayakidhi ramani ambazo tunazo, ni vizuri tukapeana nafasi na naamini na yeye mwenyewe akiona ramani pendekezwa ataafiki kwamba ni vizuri majengo yale yakatafutiwa kazi nyingine, lakini sisi tungependa tujenge hospitali ya wilaya yenye hadhi ya kulingana na Mheshimiwa Mbunge ambaye anatoka Tunduma.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. AGNESS M. MARWA aliuliza:- Kumekuwa na tatizo kubwa la dawa katika Hospitali ya Manyamanyama iliyoko Wilayani Bunda na hii ni kutokana na hospitali hiyo kutokuwa na hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya:- (a) Je, ni lini Serikali itaipa Hospitali ya Manyamanyama Hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya ili kuongeza mgao wa dawa na kupunguza shida kubwa wanayoipata wananchi? (b) Je, ni lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika hospitali hiyo ili kuongeza ufanisi?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa matatizo yaliyoko kule Manyamanyama hayana tofauti sana na matatizo yaliyoko kwenye Jimbo la Geita. Mwaka jana mwezi Machi, Waziri wa Afya alikipandisha Kituo cha Afya Nzela na kuwa hospitali ya wilaya kwa kuwa Wilaya ya Geita haina hospitali ya wilaya lakini kumekuwa na mkanganyiko kati ya TAMISEMI na Wizara ya Afya na Waziri hajawahi kutembelea eneo lile akaliona pengine akawa na huruma kama alivyopata huruma ya Waziri wa Afya. Je, ni lini Waziri wa TAMISEMI ataambatana na mimi kwenda kuona kituo kile kilichopandishwa hadhi na majengo na ubora ulioko pale ili aweze kuridhia na mambo yaende mbele? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nipongeze majibu mazuri ya Naibu wangu, Mheshimiwa Kandege aliyoyatoa katika maswali ya awali yaliyojitokeza, hata hivyo, naomba kujibu swali la mtani wangu Mheshimiwa Musukuma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuambatana, namwomba Mheshimiwa Mbunge kwanza aondoe hofu, kama tulivyokwenda katika Jimbo lake na katika Mkoa wa Geita mara nyingi na kufanya kazi kubwa sana, nimwambie mara baada ya Bunge hili la bajeti nitaomba twende kwa ziara maalum kwa sababu Mkoa wa Geita miongoni mwa mambo tunayokwenda kuyafanya ni ujenzi wa hospitali zingine za wilaya katika mkoa huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina kila sababu kufika Geita kuangalia maeneo muafaka wapi tutajenga hospitali hizo kwa manufaa mapana ya watani zangu Wasukuma wa Mkoa wa Geita ili waweze kupata huduma nzuri ya afya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Musukuma asihofu tutaondoka pamoja. (Makofi)

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESS M. MARWA aliuliza:- Kumekuwa na tatizo kubwa la dawa katika Hospitali ya Manyamanyama iliyoko Wilayani Bunda na hii ni kutokana na hospitali hiyo kutokuwa na hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya:- (a) Je, ni lini Serikali itaipa Hospitali ya Manyamanyama Hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya ili kuongeza mgao wa dawa na kupunguza shida kubwa wanayoipata wananchi? (b) Je, ni lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika hospitali hiyo ili kuongeza ufanisi?

Supplementary Question 4

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kutupa fedha kwa ajili ya upanuzi wa Kituo cha Afya cha Bahi. Kituo hiki kinawahudumia wananchi wengi sana kwa sababu mji ule unaendelea kupanuka kila siku.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo tulilonalo, upanuzi unafanyika lakini hatuna vitendea kazi, watumishi walioko pale ni Manesi wanne tu na yuko Daktari mmoja na Matabibu wachache sana ambao hawakidhi mahitaji ya wagonjwa wanaokwenda katika kituo kile cha afya. Ni lini sasa Serikali italeta watumishi na vitendea kazi vya kutosha kwa ajili ya huduma za Kituo cha Afya cha Bahi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, naomba nimshukuru Mheshimiwa Bura kwa sababu yeye amekuwa Msemaji wa Mkoa wa Dodoma kwa nafasi yake ya Viti Maalum na anautendea haki sana mkoa huu. Naomba ku-declare interest, jengo ambalo tumemaliza hivi sasa katika Hospitali ya General, amefanya kazi kubwa sana kuhakikisha tumepeleka pesa na hivi sasa tumepeleka karibuni shilingi bilioni mbili hospitali ile inapata huduma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, eneo la Bahi kweli tumeboresha kituo kile cha afya lakini siyo hivyo tu kwa kelele zake na za Mbunge wa Bahi mwaka huu tunakwenda kuanza ujenzi wa hospitali mpya za Wilaya za Bahi, Chemba pamoja na Chamwino. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hilo, wenzetu kupitia Utumishi kabla ya Juni, kuna mpango mkakati kupata watumishi wapya katika sekta ya elimu na sekta ya afya. Pia kwa vile tunajua Bahi ni pumulio la makao makuu yetu ya nchi kwa maana ya hapa Dodoma tutajitahidi kuhakikisha tunawapeleka watumishi wa kutosha ikiwa lengo kubwa ni wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)

Name

Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. AGNESS M. MARWA aliuliza:- Kumekuwa na tatizo kubwa la dawa katika Hospitali ya Manyamanyama iliyoko Wilayani Bunda na hii ni kutokana na hospitali hiyo kutokuwa na hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya:- (a) Je, ni lini Serikali itaipa Hospitali ya Manyamanyama Hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya ili kuongeza mgao wa dawa na kupunguza shida kubwa wanayoipata wananchi? (b) Je, ni lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika hospitali hiyo ili kuongeza ufanisi?

Supplementary Question 5

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Bunge lililopita nilisimama hapa nikauliza juu ya support ya Serikali katika ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kasu, nikajibiwa kwamba siyo muda mrefu pesa zitapelekwa zaidi ya shilingi milioni 500. Nataka kujua, ni lini Serikali sasa itapeleka pesa hizo maana nimetoka Jimboni bado hatujazipokea pesa hizo? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ahadi ya Serikali kupeleka pesa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kasu ni mara pesa itakapopatikana kwa sababu ni ahadi ambayo tumeiweka na tuko very firm katika hilo. Tutahakikisha katika mgao wa awamu inayofuata na kituo chake cha afya kinapata mgao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama hiyo haitoshi, katika wilaya ambazo zinaenda kujengewa hospitali za wilaya ni pamoja na wilaya yake. Kwa hiyo, naamini adha ambayo wananchi wa Nkasi wamekuwa wakiipata kuhusiana na suala zima la matibabu litapungua muda siyo mrefu sana.