Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 21 2018-04-05

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNESS M. MARWA aliuliza:-
Kumekuwa na tatizo kubwa la dawa katika Hospitali ya Manyamanyama iliyoko Wilayani Bunda na hii ni kutokana na hospitali hiyo kutokuwa na hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya:-
(a) Je, ni lini Serikali itaipa Hospitali ya Manyamanyama Hati rasmi ya kuwa Hospitali ya Wilaya ili kuongeza mgao wa dawa na kupunguza shida kubwa wanayoipata wananchi?
(b) Je, ni lini Serikali itaongeza Waganga na Wauguzi katika hospitali hiyo ili kuongeza ufanisi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agness Mathew Marwa, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Manyamanyama hakijakidhi vigezo vya kupewa hati ya kuwa Hospitali ya Wilaya kwa kuzingatia mapendekezo yaliyotolewa na timu ya ukaguzi kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto uliofanyika mwaka 2015.
Mheshimiwa Naibu Spika, upungufu uliobainika ni pamoja na ukosefu wa jengo la utawala; jengo la huduma za mionzi; jengo la kliniki ya macho; jengo la huduma za dharura; jengo la kufulia; ujenzi wa wodi ya upasuaji ya wanaume na wanawake; jengo la ufundi wa vifaa vya hospitali kwa maana (karakana); jengo la kuhifadhia maiti na nyumba za watumishi. Hivyo, kituo hicho kitapata hadhi ya kuwa hospitali endapo miundombinu yote inayohitajika itakamilika ili huduma za msingi zenye hadhi ya hospitali ziweze kutolewa.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, mahitaji ya watumishi wa afya katika Kituo cha Afya Manyamanyama ni 165, watumishi waliopo ni 78 na upungufu ni watumishi 87. Katika mwaka wa fedha 2017/2018, kituo kimepokea watumishi watano (5) akiwemo Daktari mmoja. Katika mwaka wa fedha 2018/2019, Halmashauri imeomba kibali cha kuajiri watumishi wa afya 48 ili kupunguza pengo hilo.