Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Mtambula, Idunda, Itandula, Kiyowela, Idete, Maduma na Nyololo Shuleni?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; katika awamu ya pili ya REA ambayo imekwisha kuna vijiji ambavyo havijapitiwa na katika upelekaji wa umeme ule ulienda kwenye makao makuu ya kata. Kwa mfano, pale Malangali Vijiji vya Isinikini, Kingege, Ibangi na Ikaning’ombe pale bado havijapata umeme. Je, Serikali itarudi kwenye kutekeleza ile ambayo ilikuwa ni awamu ya pili?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Serikali ilisema kwamba itapeleka umeme kwenye vituo vya afya, zahanati, pamoja na shule za sekondari na shule za msingi, lakini mpaka sasa hivi shule za msingi bado hatujaona programu kwamba, Serikali inapeleka. Je, katika awamu hii ya tatu mnatuhakikishia kwamba, katika maeneo haya niliyoyataja watapewa umeme?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme utekelezaji wa miradi ya umeme unafanana sana na miradi ya maji. Katika utekelezaji wa miradi ya umeme Wilaya zote kwa sasa wanafungua Ofisi za TANESCO. Awamu ya pili amesema kwamba, kuna vijiji ambavyo vimeachwa, kama tayari Ofisi ya TANESCO iko pale, basi wale ambao hawajapata wapeleke maombi kwenye zile ofisi ambazo zitaendelea kufanya extension ikiwa ni pamoja na kuingiza umeme kwenye majumba ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, vivyo hivyo, Taasisi za Serikali naomba sana Mheshimiwa Mbunge kwamba, kukishakuwa na ofisi ni vema hizo taasisi za Serikali kama zina mahitaji ya umeme na ni lazima zina mahitaji ya umeme, basi ni kuwasiliana na ofisi zilizopo jirani kupeleka maombi, ili waweze kufikiriwa kupelekewa umeme kwenye hizo taasisi. Kama bajeti itakuwa haitoshelezi kwenye ofisi za Wilaya au Mkoa wao basi wata-forward moja kwa moja hayo mahitaji Makao Makuu ya TANESCO ili waweze kupatiwa pesa au waweze kuingiza hizo shule na taasisi za Serikali ziweze kuingizwa katika mradi mkubwa. (Makofi)