Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 55 Energy and Minerals Wizara ya Madini 456 2017-06-28

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata za Mtambula, Idunda, Itandula, Kiyowela, Idete, Maduma na Nyololo Shuleni?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI (K.n.y. WAZIRI WA NISHATI NA MADINI) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi kabambe wa usambazaji umeme vijijini awamu ya tatu umeanza kwa nchi nzima tangu mwezi Machi, 2017. Mradi huu utajumuisha vipengele-mradi vitatu vya Densification, Grid Extension na Off-Grid Renewable ambayo inalenga kuongeza wigo wa usambazaji umeme katika vijiji na vitongoji ambavyo havikufikiwa na miundombinu ya umeme. Kata za Idete, Idunda, Itandula, Kiyowela, Mtambula, Maduma pamoja na Kata nyingine za Wilaya ya Mufindi zimejumuishwa katika utekelezaji wa mradi wa REA awamu ya tatu wa Grid Extension utakaokamilika mwaka wa fedha 2020/2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji vya kata hizo itahusisha ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 153.65; ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4, yenye urefu wa kilometa 233; ufungaji wa transfoma 92, pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 3,225. Gharama ya kazi hii ni shilingi bilioni 14.1. (Makofi)