Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA (K.n.y. MHE. DOTO M. BITEKO) aliuliza:- Je, ni kwa nini Serikali ilihamisha madaktari saba kwa mara moja kutoka Hospitali ya Wilaya ya Bukombe huku ikijua Wilaya ya Bukombe ina upungufu mkubwa wa madaktari?

Supplementary Question 1

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwanza nitoe shukrani kwa kupeleka madaktari wanane kwa awamu, watano halafu watatu. Hata hivyo, kuna tetesi kwamba kuna daktari mmoja atahamishwa hivi karibuni. Napenda kujua kama ni kweli na kama siyo kweli basi nipate ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Waziri kwamba kama wakimhamisha yule watatuletea tena lini daktari mwingine? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa changamoto katika Hospitali ya Wilaya ya Bukombe ni sawa kabisa na changomoto iliyoko katika Halmshauri ya Wilaya ya Geita, tuna upungufu mkubwa sana wa madaktari pamoja na wauguzi. Je, Serikali inasemaje kuhakikisha kwamba Serikali inaleta watumishi wa afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, suala la kwamba kuna tetesi za kuhamishwa hivi karibuni kwa daktari mwingine labda kwa sababu anajua ambayo Waheshimiwa Wabunge wengi hawajui na labda pengine kwa sababu ya kuweka sawa niweke vizuri kwamba hata ule uhamisho wa mwanzo tulioufanya ulikuwa ni kwa sababu kulikuwa kuna shida ya kutafuta madaraka hali iliyopelekea daktari mmoja aliyekuwa anakaimu nafasi ile akashambuliwa mtaani ambapo ilionekana kama ni kutokana na mazingira hayo. Ndiyo maana tukafanya ule uhamisho na baadaye tukapeleka madaktari wengine. Kwa hiyo, kama ni tetesi zenye dhana ile ile na pengine hatua hizi zitakuwa zina sababu ile ile atahama, lakini haina maana kwamba hatutapeleka daktari mwingine kuziba nafasi hiyo.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameuliza kuhusu upungufu wa madaktari kwa maeneo yote sasa siyo tu Bukombe na Geita, lakini pia najua tuna upungufu wa madaktari na wauguzi katika maeneo mengi. Mheshimiwa Rais ametoa kibali cha ajira za watumishi wengine 15,000 ambao wataziba nafasi ya hawa watumishi hewa waliokuwa na vyeti fake ambao wameondolewa. Kibali hicho kinaendelea na katika kibali hicho pia tuna idadi kubwa tu ya wataalam wa afya ambao watakuja kwa ajili ya ku-replace lakini tuna ajira zingine 54,000 ambazo ni za mwaka huu wa fedha ambazo na zenyewe tunaamini katika kufanya hivyo tutaziba eneo kubwa sana la upungufu siyo tu wa idara hii ya afya lakini pia na idara nyingine kwa ujumla wake.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA (K.n.y. MHE. DOTO M. BITEKO) aliuliza:- Je, ni kwa nini Serikali ilihamisha madaktari saba kwa mara moja kutoka Hospitali ya Wilaya ya Bukombe huku ikijua Wilaya ya Bukombe ina upungufu mkubwa wa madaktari?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sasa kutokana na vyeti feki vimeondoa kabisa watumishi wa afya katika zahanati zetu. Je, ni lini hasa hawa watumishi wataenda kuajiriwa yaani wanayo time frame kwa sababu sasa hivi zahanati zina shida katika huduma hii ya afya? Ahsante sana. (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kutokana na vyeti fake, watumishi takribani 12,000 wameondolewa katika utumishi wa umma.
Hata hivyo, kibali kilichotolewa na Mheshimiwa Rais ni cha watumishi 15,000 na tunaamini kabisa kwamba hawa watakwenda kuziba. Mchakato wake ilibidi kwanza tufanye uhakiki mzuri kwamba waliotoka ni wa idara zipi na zipi, walimu ni wangapi, manesi wangapi na madaktari wangapi. Kazi hiyo tumeimaliza na tumeshakabidhi Wizara ya Utumishi na mchakato unaendelea. Bila shaka wakati wowote tunaweza tukawaingiza katika ajira watumishi hawa wapya.