Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 7 Sitting 44 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 361 2017-06-08

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA (K.n.y. MHE. DOTO M. BITEKO) aliuliza:-
Je, ni kwa nini Serikali ilihamisha madaktari saba kwa mara moja kutoka Hospitali ya Wilaya ya Bukombe huku ikijua Wilaya ya Bukombe ina upungufu mkubwa wa madaktari?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ilihamisha madaktari sita katika Hospitali ya Wilaya ya Bukombe ikiwa ni utaratibu wa kawaida wa kuimarisha ufanisi katika utoaji wa huduma za afya kwa wagonjwa. Ili kuziba nafasi za waliohamishwa kwa lengo la kutoathiri utoaji wa huduma za afya hospitalini hapo, Halmashauri hiyo ilipelekewa madaktari wapya watano na badaye Serikali ilipeleka madaktari wengine watatu na kufanya jumla ya madaktari waliopelekwa Bukombe kuwa nane. Lengo lilikuwa ni kuboresha utoaji wa huduma katika hospitali hiyo.