Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA (K. n. y. MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA) aliuliza:- Tangu kutangazwa sheria ya kuzitaka Halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake na vijana. Je, ni nini kinaifanya Serikali kutokuwa na taarifa ya mfuko huo kujua una kiasi gani cha fedha?

Supplementary Question 1

MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nitakuwa na swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Halmashauri nyingi zimekuwa hazitengi fedha hizi kwa ajili ya vijana na akina mama; lakini vile vile tuna tatizo sasa hivi ambalo tungekuwa makini zaidi kuliangalia suala la ndugu zetu walemavu, kwamba kuweze kuwa na uwezekano sasa wa kuzitenga fedha kutoka katika hizi asilimia 10 kwa ajili ya walemavu, vijana na akina mama.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa sababu majibu ya msingi yameshatolewa ningependa kufahamu kwa hizi Halmashauri ambazo kwa ujumla zimeshindwa kutenga fedha hizi kwa ajili ya vijana kama mimi akina mama; na kama tulivyoongea kuhusu walemavu ningependa kufahamu sasa.
Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba inazibana halmashauri hizi ili ziweze kupata mapato ya ndani kwa uhakika na kuhakikisha kwamba inatenga fedha hizi kwa ajili ya makundi haya? Nakushukuru.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. GEORGE J. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa swali la nyongeza ambalo linawagusa akina mama na vijana nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kupitia Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI ameshatoa waraka tangu mwaka jana mwezi wa saba kuelekeza Halmashauri zote nchini kuhakikisha kwamba wanatenga asilimia 10 kwa ajili ya mikopo ya vijana na wanawake na hilo ndiyo maana nimesema hapa kupitia Bunge lako Tukufu kwamba ni lazima watenge na wasipotenga sasa Serikali itaanza kuchukua hatua za kiutumishi dhidi ya Wakurugenzi ambao hawatengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni kwa sababu kinachotakiwa kufanyika ni kutenga kile ambacho kimekusanywa, kama kimekusanywa bilioni 10 basi asilimia 10 ya bilioni 10 lazima itengwe kwa ajili ya wanawake na vijana. (Makofi)

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA (K. n. y. MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA) aliuliza:- Tangu kutangazwa sheria ya kuzitaka Halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake na vijana. Je, ni nini kinaifanya Serikali kutokuwa na taarifa ya mfuko huo kujua una kiasi gani cha fedha?

Supplementary Question 2

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Na mimi naomba kuuliza swali la nyongeza kuwa hili suala la kutenga asilimia 10 wa ajili ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu linaonekana kama halijakaa kisheria sana na ndiyo maana wakati mwingine wanatumia hiyo loopholes za kuepuka kutenga hilo fungu.
Je, Serikali ina mkakati wowote wa kuhakikisha kuwa sheria au kanuni zinarekebishwa ili kuhakikisha kuwa hili jambo linakuwa kisheria zaidi? Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. GEORGE J. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nilijulishe Bunge lako Tukufu kwamba tumeshapokea maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu pendekezo la kupitia upya sheria ambayo ndiyo tunaiangalia ambayo ilikuwa ndio misingi wa kuanzishwa hii mifuko ili tuweze kuona kwamba tunaweza kurekebisha sehemu gani ili kuweze kuzibana zaidi Halmashauri kuhusu kutenga asilimia 10.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA (K. n. y. MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA) aliuliza:- Tangu kutangazwa sheria ya kuzitaka Halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake na vijana. Je, ni nini kinaifanya Serikali kutokuwa na taarifa ya mfuko huo kujua una kiasi gani cha fedha?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa fedha hizi zimeleta mgogoro sana zinapowekwa kwenye akaunti ya pamoja, je, Serikali haioni haja sasa kuzielekeza Halmashauri kuanzisha akaunti maalum kwa ajili ya hii asilimia 10 peke yake? Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. GEORGE J. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuliahidi Bunge lako Tukufu kwamba tumechukua maoni ya Mheshimiwa Sima ambayo naamini ni maoni ya Waheshimiwa Wabunge wote na tutalifanyia kazi.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA (K. n. y. MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA) aliuliza:- Tangu kutangazwa sheria ya kuzitaka Halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake na vijana. Je, ni nini kinaifanya Serikali kutokuwa na taarifa ya mfuko huo kujua una kiasi gani cha fedha?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa vipo vikundi vya akina mama ambavyo vimeanzishwa na kuunda SACCOS, lakini halmashauri hawatoi pesa hiyo asilimia 10 kuvipatia vikundi hivyo na wakati vikundi hivyo havijaweza kukopeshwa na mabenki au taasisi mbalimbali za kifedha.Je, ni kwa nini sasa Serikali isiagize Halmashauri ili vikundi hivyo navyo vilivyoundwa kama SACCOS viweze kukopeshwa pesa hiyo? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. GEORGE J. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Genzambuke kwa kuzidi kuvijali vikundi vya SACCOS ambavyo vimeanzishwa kwenye Halmashauri nyingi hapa nchini ikiwemo Halmashauri ya Kasulu pale anakotoka.
Hili suala ni wazo zuri na mimi naomba sana sana badala ya kulijibu hapa haraka haraka tulichukue tukalifanyie kazi zaidi kwa sababu malengo Mfuko wa Vijana na Wanawake ni kukopesha wale vijana ambao wanajishughulisha na kazi za uzalishaji mali moja kwa moja. Sasa hili suala la kusema kwamba tuwakopeshe halafu na wao wakopeshane ni wazo jipya ambalo linahitaji kujadiliwa zaidi kitaalam ili tuweze kutoa maelekezo. Ahsante sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WALEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba tu niliarifu tu Bunge lako Tukufu kwamba pamoja na kuendelea kulifanyia kazi jambo hili naomba kuendelea kuwakumbusha Waheshimiwa Wabunge kuwa katika kutoa mikopo kwa vijana kupitia Mfuko wa Vijana wa asilimia tano, zile zinazotengeneza asilimia 10 kwenye Halmashauri tayari Serikali ilishagiza vijana kupitia halmashauri zao waunde SACCOS za vijana ili waweze kunufaika na mikopo hiyo na kupitia kwenye hizo SACCOS waweze kujikopesha na mikopo hiyo iwe revolving. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo pamoja na vijana ni lazima pia kuwaangalia na akina mama. Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu na hasa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi limeanza kuweka mkakati maalum wa kuhakikisha linafikia vikundi vya VICOBA na SACCOS za wanawake na vijana katika nchi nzima ya Tanzania. Nimuombe sana Mheshimiwa Genzabuke, kwa kuwa kupitia Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi tuna mifuko takribani 17 ya kuwawezesha wananchi Mheshimiwa Genzabuke awasiliane na mimi tuwaelekeze akina mama hawa wa Kigoma wanaweza wakasaidiwaje. (Makofi)