Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:- Kumekuwa na idadi kubwa ya ajali nchini zinazosababisha vifo, majeruhi na upotevu wa mali:- • Je, kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia 2016 – 2018 ni ajali ngapi zimetokea na kusababisha vifo au majeruhi? • Je, ni waathirika wangapi waliomba fidia na wangapi mpaka sasa wamelipwa fidia zao kutoka kampuni za bima?

Supplementary Question 1

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mheshimiwa Waziri mimi nilikuwa very specific kwenye swali langu la msingi, niliuliza ni watu wangapi waliomba fidia na wangapi wamelipwa mpaka sasa hivi. Kwa maelezo yako Mheshimiwa Waziri inaonesha jumla ya vifo na majeruhi ni zaidi ya elfu 14, hiyo ni kwa mwaka 2016 mpaka 2018 na ambao wamelipwa fidia mpaka sasa hivi ni watu 1,583, ni kama asilimia zaidi ya 10 kidogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe kuwa mwaka 2009 Bunge lilipitisha Sheria namba 10 ili kuwalinda waathirika wa ajali hizo. Sasa Mheshimiwa Waziri hawa wenzetu ambao wanaoshughulikia hili suala la bima hawa wenzetu wa TIRA (Tanzania Insurance Regulatory Authority) inaonesha kabisa kuna upungufu. Ambao wamekuwa beneficiary wakubwa wa hii issue ya bima ni hizi kampuni ambazo yanakatisha bima, lakini ajali inapotokea inaonesha kabisa Watanzania wamekuwa ni waathirika wakubwa ambao wameachiwa mzigo mkubwa. Sasa Mheshimiwa Waziri huoni ni wakati muafaka sasa tuanzishe idara maalum ambayo itakuwa inatoa elimu kwa Watanzania pale ajali inapotokea ili wajue hatua stahiki ambazo wanatakiwa kuchukua ili walipwe fidia zao? Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Rose Tweve kwa ku-take serious concern ya Watanzania wanaopata matatizo hayo na kutokupata fidia ama kuchelewa kupata fidia. Niseme tu kama Serikali tunapokea wazo lake na kwa sababu tuna wataalam wazo hilo litachambuliwa kitaalam.
Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe rai kwa Watanzania kuchukua hatua haraka za kufuata taratibu zinazotakiwa badala ya utaratibu ambao maeneo mengi wamekuwa wakifanya panapotokea matatizo ya aina hiyo; kuamua kuchukua sheria mikononi ama kuamua kufanya taratibu za njia za mkato ambazo zinasababisha wao kukosa kile ambacho walitakiwa wapate.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:- Kumekuwa na idadi kubwa ya ajali nchini zinazosababisha vifo, majeruhi na upotevu wa mali:- • Je, kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia 2016 – 2018 ni ajali ngapi zimetokea na kusababisha vifo au majeruhi? • Je, ni waathirika wangapi waliomba fidia na wangapi mpaka sasa wamelipwa fidia zao kutoka kampuni za bima?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa kuweza kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa hizi ajali za barabarani zinatokana na uzembe wa baadhi ya madereva na baadhi ya madereva kutumia simu wakati wakiwa wanatumia vyombo ya moto. Je, Serikali ina mkakati gani wa kurekebisha Sheria ya Usalama Barabarani ili kuwachukulia hatua kali zaidi hawa madereva ambao wamekuwa wakitumia simu wakati wakitumia vyombo vya moto? Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba kweli kuna kiwango kikubwa cha ajali zinatokea kutokana na uzembe. Ukiangalia hata kwenye kumbukumbu zaidi takribani ya matukio zaidi ya 1,500 yanatokana na uzembe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kile alichokisema cha kurekebisha sheria na kuchukua hatua tunaendelea na utaratibu huo na tunasema tunakokwenda tutaanza hata kutumia taratibu ambazo nchi zingine wanatumia kwa ku- count down dereva ambaye anapatikana sana na makosa aweze kukosa sifa za kuendelea kumiliki leseni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunalifanyia kazi wazo lake na nimpongeze sana kwa kuguswa na jambo hili kwa sababu limekuwa likisababisha hasara sana kwa familia na kwa Taifa. (Makofi)

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:- Kumekuwa na idadi kubwa ya ajali nchini zinazosababisha vifo, majeruhi na upotevu wa mali:- • Je, kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia 2016 – 2018 ni ajali ngapi zimetokea na kusababisha vifo au majeruhi? • Je, ni waathirika wangapi waliomba fidia na wangapi mpaka sasa wamelipwa fidia zao kutoka kampuni za bima?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri ambayo anaifanya. Swali langu ni hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, ajali zinaendelea kutokea kwa wingi, hata hivi sasa hivi ninavyoongea ukipita barabara ya Morogoro – Dodoma kuna ajali nyingi sana, lakini traffic wamegeuka agent wa TRA kazi yao ni kusimamisha magari na kutoza faini. Sasa Mheshimiwa Waziri naomba atoe tamko kuanzia leo hii matrafiki waache kutoza faini wakazane na kutoa elimu kwa kutoa elimu kwa watumia vyombo vya moto na wasafiri ili wajue ni haki gani watapata pindi ajali zinapotokea. (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, moja, sisi kama Wizara ya Mambo ya Ndani na Jeshi la Polisi, kutoza faini ama kukusanya faini si kipaumbele chetu; sisi kipaumbele chetu ni maisha ya Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuwa imepita miaka mingi sana ya kutoa elimu na tunaendelea kuona kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge alisema uzembe bado uko mwingi sana ndipo tunapokwenda kwenye hatua hiyo ya kutoza faini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kama Watanzania watazingatia kwamba wamebeba dhamana kubwa ya maisha ya Watanzania na maisha yao wao wenyewe, wakawa waangalifu hili suala la faini litakuwa limeisha, lakini kwa kuwa tunawapenda zaidi na tunapenda zaidi maisha yao ndiyo maana tunakuwa hatuna njia nyingi zaidi ya kuchukua sheria kali ili kuweza kuokoa maisha yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nitoe rai kwa Jeshi la Polisi kuendelea kuwa strictly, kuendelea kuwa wakali punde watu wanapofanya mzaha na huku wakiwa wamebeba abiria ili kuweza kuokoa maisha yanayopotea kutokana na ajali nyingi zinazotokea barabarani. Jambo hili ninalolisemea ni kwa vyombo vya moto vyote, ukianzia magari ambayo si ya abiria pamoja na bodaboda.
Mheshimiwa Naibu Spika, nalisisitiza sana hili kwa sababu tumeshuhudia vifo vikiwa vimetokea na pale tunapokwenda kwenye kuokoa miili tunakuta watu walikuwa tayari walishaandikiwa faini ikiwa ni kwamba wameambiwa kwamba wanakwenda mwendo kasi. Hata hivyo, pamoja na faini wanaendelea na mwendo kasi ama na uzembe na baadaye inagharimu maisha ya Watanzania.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:- Kumekuwa na idadi kubwa ya ajali nchini zinazosababisha vifo, majeruhi na upotevu wa mali:- • Je, kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia 2016 – 2018 ni ajali ngapi zimetokea na kusababisha vifo au majeruhi? • Je, ni waathirika wangapi waliomba fidia na wangapi mpaka sasa wamelipwa fidia zao kutoka kampuni za bima?

Supplementary Question 4

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kuuliza swali. Kwa kuwa kuna upungufu mkubwa wa askari katika baadhi ya sehemu na askari wengi sana kwa maana ya traffic wako barabaran, je, Serikali sasa haioni imefikia wakati wa kuweza kupata kamera au teknolojia nyingine badala ya kutumia askari ambao kwa kweli utendaji wao hauna tija. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Mwamoto kwa jambo hilo alilolitoa. Ni kweli kuna uhitaji mkubwa sana wa kuhamia kwenye teknolojia, nchi nyingi zilizoendelea ndio utaratibu unaotumika. Sisi kama Serikali wataalam wanaendelea kufanyia kazi jambo hilo ikiwepo na kufanya upembuzi yakinifu ili kuweza kujua mahitaji pamoja na maeneo ambayo tunaweza tukaanza nayo ili kuweza kupunguza adha inayojitokeza; kwa sababu kwanza tu kukaa kwenye jua kukaa kwenye mvua pamoja na uchache wa askari inasababisha ufanisi kupungua.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, jambo lake hilo tunalifanyia kazi na nimpongeze sana kwa kuleta hoja hiyo makini, lakini nimpe pole tu kwa yeye ni ndugu yangu kwa yale yaliyotokea Jumamosi, yaliyotokea tarehe moja. (Makofi) Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.