Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 07 2018-04-03

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:-
Kumekuwa na idadi kubwa ya ajali nchini zinazosababisha vifo, majeruhi na upotevu wa mali:-
• Je, kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia 2016
– 2018 ni ajali ngapi zimetokea na kusababisha vifo au majeruhi?
• Je, ni waathirika wangapi waliomba fidia na wangapi mpaka sasa wamelipwa fidia zao kutoka kampuni za bima?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rose Tweve, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
• Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa katika kipindi cha mwaka 2016 hadi 2018 Jeshi la Polisi kupitia Kikosi cha Usalama Barabarani lilichukua hatua za makusudi kupunguza ajali ambapo mpaka kufikia Disemba, 2017 limefanikiwa kupunguza ajali za barabarani kwa asilimia 43.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2016 kulitokea jumla ya ajali 9,856 ambazo zilisababisha vifo 3,256 na majeruhi 2,128. Mwaka 2017 kulitokea ajali 5,310 ambazo zilisababisha vifo 2,533 na majeruhi 5,355 wakati kwa kipindi cha Januari hadi Februari, 2018 zimetokea ajali 769 ambazo zimesababisha vifo 334 na majeruhi 698.
• Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka 2016 hadi 2018 jumla ya waathirika wa ajali 1,583 walilipwa fidia yenye jumla ya thamani ya fedha za kitanzania bilioni 7.3 kutoka kampuni mbalimbali za bima.