Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Kwa muda mrefu wananchi wa Karagwe wamekuwa wakiahidiwa kujengewa Hospitali ya Wilaya na taratibu zote zimekuwa zikifuatwa kupitia Vikao vya Baraza la Madiwani na RCC lakini maombi haya hutupiliwa mbali na TAMISEMI. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa hospitali hii ambayo pia ipo kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, na pia nitumie nafasi hii kumshukuru sana kaka yangu, Mheshimiwa Selemani Jafo na Dada Jenista Mhagama. Baada ya kufika Karagwe na kukuta wilaya ambayo ina watu takribani 360,000 ina Kituo cha Afya kimoja cha Serikali waliweka nguvu na Serikali sasa imetusaidia tumekamilisha hicho Kituo cha Afya cha Kayanga, nawashukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza; swali la kwanza, kwa vile Wilaya ya Karagwe ina Kituo cha Afya kimoja cha Serikali, na hivi sasa naishukuru TAMISEMI tunaenda kukamilisha Kituo cha Afya cha Nyakayanja, mnaonaje wakati mchakato wa kujenga Hospitali ya Wilaya unaendelea mtupe angalau vituo vya afya viwili ili ku-balance jiografia ya Karagwe?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa TAMISEMI na Wizara ya Afya wanafanya kazi nzuri, mnaonaje mkae na development partners kwa sababu Kamati ya Huduma za Jamii inaonesha kwamba kuna Wilaya 67 katika nchi yetu ambazo bado hazina Hospitali za Wilaya. Sasa kwa sababu Serikali inafanya kazi nzuri ya kutoa huduma mnaonaje mkae na development partners ili mtengeneze proposal ambayo itatusaidia kukamilisha ujenzi wa Hospitali 67 za Wilaya? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza ndugu yangu, Mheshimiwa Bashungwa kwa jinsi ambavyo anapigana katika jimbo lake kuhakikisha kwamba wananchi wake wanapata huduma ya afya iliyo bora. Katika maelezo yake anaongelea kwamba kuna kituo cha afya kimoja, ni kiu yake kwamba vituo vya afya vingeongezeka walau viwili tena.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba vituo vya afya vinajengwa katika maeneo yote na kwa kufuata uwiano sawia. Kwa hiyo, katika awamu inayokuja naomba nimhakikishie kwamba walau tutahakikisha kwamba kituo kingine cha afya kinapelekwa kule haraka iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili anauliza uwezekano wa Serikali kushirikiana na development partners katika kuhakikisha kwamba tunaenda kumaliza tatizo la ujenzi wa Hospitali za Wilaya. Ni nia ya Serikali na milango iko wazi kwa yeyote yule ambaye ana nia njema ya kusaidia Serikali katika ujenzi wa Hospitali za Wilaya, tunamkaribisha, ilimradi katika yale masharti ambayo yatakuwa si ya kudhalilisha nchi yetu, sisi kama Serikali tuko tayari.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Kwa muda mrefu wananchi wa Karagwe wamekuwa wakiahidiwa kujengewa Hospitali ya Wilaya na taratibu zote zimekuwa zikifuatwa kupitia Vikao vya Baraza la Madiwani na RCC lakini maombi haya hutupiliwa mbali na TAMISEMI. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa hospitali hii ambayo pia ipo kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mkoa wa Tabora Wilaya mbili hazina Hospitali za Wilaya, Sikonge na Tabora Manispaa na viwanja tayari vipo, je, Serikali inasema nini? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la la Mheshimiwa Mwanne Mchemba, ambaye wakati tumefanya ziara kwenda Kilolo yeye ndio alikuwa Mwenyekiti wa Kamati na akashuhudia kazi njema ambayo inafanywa na Serikali, Hospitali ya Wilaya ya Kilolo itakuwa miongoni mwa hospitali za kutilia mfano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa katika swali lake anasema Serikali inasema nini kuhusiana na Wilaya mbili za Sikonge na Tabora Mjini ambazo hazina Hospitali za Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu katika majibu yangu ya mwanzo, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo hakuna hospitali za wilaya zinajengwa ili kupunguza mlundikano wa wagonjwa kwenda katika Hospitali za Rufaa ili wale ambao wanaweza kutibiwa katika Hospitali za Wilaya waweze kutibiwa. Naomba niiombe Halmashauri, ni vizuri na wao wakaonesha kwamba ni hitaji la wananchi kwa hiyo na wao katika vyanzo vyao vya mapato waanze pia ujenzi ili na Serikali Kuu tuweze kushirikiana nao.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:- Kwa muda mrefu wananchi wa Karagwe wamekuwa wakiahidiwa kujengewa Hospitali ya Wilaya na taratibu zote zimekuwa zikifuatwa kupitia Vikao vya Baraza la Madiwani na RCC lakini maombi haya hutupiliwa mbali na TAMISEMI. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa hospitali hii ambayo pia ipo kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 3

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu la Tunduma na Wilaya yetu ya Momba kulikuwa na majengo ambayo yalikuwa yanatumika na Kampuni ya CC iliyokuwa inajenga barabara ya kutoka Tunduma kwenda Sumbawanga. Majengo hayo yaliteuliwa kwamba yangeweza kutumika kama Hospitali ya Wilaya, lakini sasa hivi inaonesha kuna mabadiliko. Waziri anawaambia nini wananchi wa Mji wa Tunduma kuhusiana na majengo yale kwa sababu aliwahakikishia kwamba itakuwa Hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza nitaenda kufanya follow up kujua kwamba ni Waziri gani alitoa commitment hiyo.
Jambo la pili, nafahamu wazi kwamba kuna maeneo mengi sana majengo yaliyokuwa yakitumika na wenzetu wa Wizara ya Ujenzi, hasa yale makampuni, majengo yale mengi sana yameombwa kwa ajili ya ama vituo vya afya au maendelezo ya Hospitali za Wilaya. Ninafahamu wazi kwamba Tunduma kuna changamoto kubwa kwa sababu idadi ya watu pale ni kubwa na ndiyo maana tunaanza ule ujenzi wa kituo cha afya, japokuwa umekuwa ukisuasua lakini tutasimamia kwa karibu ili uweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo hilo ndugu yangu Mheshimiwa Mwakajoka naomba niseme kwamba tunalichukua kwenda kulifanyia tathmini kuona nini kimekwamisha, kwa sababu hatimaye tunataka wananchi wa Tunduma wapate huduma vyema kabisa. Kwa hiyo tutalifanyia kazi Serikali kwa ujumla wake wote.