Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 110 2018-02-09

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA aliuliza:-
Kwa muda mrefu wananchi wa Karagwe wamekuwa wakiahidiwa kujengewa Hospitali ya Wilaya na taratibu zote zimekuwa zikifuatwa kupitia Vikao vya Baraza la Madiwani na RCC lakini maombi haya hutupiliwa mbali na TAMISEMI.
Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa hospitali hii ambayo pia ipo kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Lugha Bashungwa, Mbunge wa Karagwe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe imetenga eneo la ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na kupitishwa kwenye vikao vya kisheria ili kutekeleza shughuli ya ujenzi. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 imetengwa shilingi milioni 70 kutoka kwenye fedha za mapato ya ndani na shilingi milioni 60 kutoka kwenye ruzuku ya miradi ya maendeleo (CDG).
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri imeweka kipaumbele na kutenga shilingi milioni mia moja ili kuendelea na ujenzi wa hospitali hiyo endapo Bunge litaridhia maombi hayo. Chanzo cha fedha hizo ni mapato ya ndani shilingi milioni 50 na shilingi milioni 50 zitatokana na ruzuku ya maendeleo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.