Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Ali Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. JUMA ALI JUMA aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi na wananchi wa Kisakasaka hali inayoleta wasiwasi kwa wananchi. (a) Je, ni lini Serikali itaupatia ufumbuzi mgogoro huo? (b) Je, kwa nini Serikali isiwaruhusu wananchi hao kuendelea na shughuli za kilimo na mifugo wakati wakisubiri ufumbuzi wa tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA ALI JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mgogoro huu ni wa muda mrefu toka mwaka 1979, viongozi mbalimbali wametembelea katika eneo lile lakini hadi leo halijapatiwa ufumbuzi. Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari mimi na yeye pamoja na viongozi wanaolizunguka lile eneo tukae pamoja ili tuupatie ufumbuzi mgogoro huu?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mgogoro huu ni wa muda mrefu na nataka nimfahamishe Mheshimiwa Juma kwamba mimi binafsi nimefika eneo hilo, nilifanya mazungumzo na uongozi wa kikosi pamoja na uongozi wa eneo na wananchi wa pale tulizungumza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, kinachokwamisha kutatua sasa hivi ni suala la fedha za kupima kwa sababu Jeshi lilisharidhia kufanya mabadiliko ya mipaka yake ili wananchi ambao sasa hivi wanaonekana wapo ndani ya eneo la kambi waweze kutolewa. Hata hivyo, nitakuwa tayari kuzungumza na Mheshimiwa Mbunge ili kumueleza zaidi ni hatua gani ambazo zinastahili kuchukuliwa kwa mujibu wa ziara niliyoifanya pale na fedha zikipatikana. (Makofi)

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. JUMA ALI JUMA aliuliza:- Kuna mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi na wananchi wa Kisakasaka hali inayoleta wasiwasi kwa wananchi. (a) Je, ni lini Serikali itaupatia ufumbuzi mgogoro huo? (b) Je, kwa nini Serikali isiwaruhusu wananchi hao kuendelea na shughuli za kilimo na mifugo wakati wakisubiri ufumbuzi wa tatizo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Moja ya matatizo makubwa makubwa ambayo tumekabiliana nayo kwa wananchi wanaozunguka Kambi ya Maji Maji kikosi Namba 41 na kikosi cha JKT katika Kata ya Mchonda ni tatizo ya migogoro ya ardhi, na tatizo hili tayari tumesharipoti kwa watu wa Wizara.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kufahamu msimamo wa Serikali au Wizara juu ya fidia ambazo wameahidi kuwalipa wananchi wale ili waweze kuachia yale maeneo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna Kambi nyingi ambazo zina migogoro ya ardhi. Kama ninavyosema mara kwa mara hapa migogoro hii iko ya aina nyingi, kuna migogoro ambayo Jeshi limechukua ardhi lakini wananchi bado hawajalipwa fidia, yapo maeneo ambayo wananchi wamevamia Kambi za Jeshi na na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninachoweza kusema hapa ni kwamba tumeweka fedha kwenye bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ili kwa yale maeneo ambayo fidia zinahitajika tuweze kulipa ili kumaliza migogoro hii, mwaka wa bajeti haujaisha na nimategemeo yetu kwamba fedha hizo zikipatikana tutatoa fidia kwa wale ambao wanastahili kupewa fidia maana wako wengine ambao wao wamevamia kambi za Jeshi hao hawatalipwa fidia. (Makofi)