Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 8 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 106 2018-02-07

Name

Juma Ali Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. JUMA ALI JUMA aliuliza:-
Kuna mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi na wananchi wa Kisakasaka hali inayoleta wasiwasi kwa wananchi.
(a) Je, ni lini Serikali itaupatia ufumbuzi mgogoro huo?
(b) Je, kwa nini Serikali isiwaruhusu wananchi hao kuendelea na shughuli za kilimo na mifugo wakati wakisubiri ufumbuzi wa tatizo hilo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Ali Juma, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, inatambua uwepo wa mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi na Wananchi katika eneo la Kisakasaka. Katika kupata ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro huu, Makao Makuu ya Jeshi iliridhia kurekebisha mpaka wa Kambi ya Kisakasaka ili kuwaachia wananchi eneo lenye mgogoro na hivyo kuleta suluhisho la kudumu kwenye mgogoro huo. Zoezi hilo halijafanyika kutokana na ufinyu wa bajeti, hata hivyo katika mwaka huu wa fedha wa 2017/2018 tunategemea kutekeleza zoezi hili.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa napenda kuwasihi wananchi wawe wastahimilivu wakati Serikali inachukua hatua stahiki ili kuzuia madhara yoyote yanayoweza kutokea kwa wananchi endapo wataendelea na shughuli za kilimo na mifugo katika eneo hilo.