Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. JAMES F. MBATIA) aliuliza:- (a) Je, kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita Mlima Kilimanjaro umeliingizia Taifa mapato ya fedha kiasi gani kwa njia ya utalii? (b) Je, ni asilimia ngapi ya mapato hayo yametumika kuweka miundombinu endelevu ya kuuhifadhi Mlima huo? (c) Je, ni asilimia ngapi ya mapato hayo yametumika katika dhana nzima ya ujirani mwema katika kutoa huduma zinazokuza utu wa wananchi wanaozungukwa na Mlima huo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu ya swali hili na niombe kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna nyakati ambazo mlima Kilimanjaro unapata ajali ya moto na kwa sababu hiyo wananchi wanaotokana na halmashauri zinazozunguka mlima wanafanya kazi ya kuzima moto huo, hususan wananchi wa Wilaya ya Rombo na kikubwa wanachoambulia ni nusu mkate. Sasa kwa kuwa kuna utaratibu wa kutoa mrabaha kwa halmashauri ambazo zina madini; je, Serikali haioni kwamba umefika wakati sasa mapato yanayotokana na mlima Kilimanjaro kiasi fulani kitolewa kama mrabaha kwa halmashauri zinazozunguka mlima ili iwe kama incentive na kuwafanya wananchi hao waweze kuulinda mlima wakati majanga ya moto yanapotokea? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuna vijana wapagazi (porters) ambao wanabeba chakula, maji, gesi na kadhalika kwa ajili ya kuwasaidia watalii kupanda mlima. Vijana hawa wana malalamiko makubwa sana kwamba malipo yao ni ya kinyonyaji. Je, Serikali iko tayari kuchunguza malalamiko haya na kuwasaidia hawa vijana ili waweze kupata stahiki zao?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza wananchi kwa jinsi ambavyo wamekuwa wakishiriki katika kuzima moto pale unapojitokeza katika hifadhi ya Kilimanjaro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mrabaha hasa kwenye Halmashauri zile ambazo zinazozunguka mlima Kilimanjaro, naomba niseme kwamba hilo tutalifanyia kazi, tutangalia kama hilo linaweza likafanyiwa kazi. Kwa utaratibu uliopo hivi sasa ni kwamba katika bajeti nzima ya hifadhi za Taifa (TANAPA) asilimia tano mpaka saba huwa zinatengwa kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali inayoibuliwa na wananchi walioko katika maeneo yaliyo jirani na hifadhi mbalimbali. Kwa hiyo, katika hili ambalo amelisema basi tutalifanyia kazi tuone kama nalo linaweza likafanyiwa kama tulivyofanya madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la kuhusu wapagazi, kama atakumbuka hapo tulipokuwa tunajibu swali lililokuwa linahusu maslahi wapagazi na waongoza utalii tulisema; katika kikao kilichofanyika Arusha kati Serikali wapagazi na vyama vyao pamoja; katika utatu huo tulikubaliana kabisa viwango ambavyo vimependekezwa na ambavyo tulifikia muafaka. Tukaagiza kwamba sasa wale wote, mashirika yote, taasisi zote, kampuni zote za kitalii lazima ziingie mikataba na hao wapagazi ili angalau kuhakikisha kwamba kwa siku kila mmoja anapata fedha zisizopungua dola elfu kumi kwa siku. (Makofi)

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. JAMES F. MBATIA) aliuliza:- (a) Je, kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita Mlima Kilimanjaro umeliingizia Taifa mapato ya fedha kiasi gani kwa njia ya utalii? (b) Je, ni asilimia ngapi ya mapato hayo yametumika kuweka miundombinu endelevu ya kuuhifadhi Mlima huo? (c) Je, ni asilimia ngapi ya mapato hayo yametumika katika dhana nzima ya ujirani mwema katika kutoa huduma zinazokuza utu wa wananchi wanaozungukwa na Mlima huo?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa mlima Kilimanjaro ni kivutio kikubwa na kinachoingiza pesa za kigeni kwa kiwango kikubwa kama kilivyotajwa. Je, ni lini sasa Serikali itaboresha miundombinu ya upandwaji wa milima huo kama inavyofanyika katika nchi zingine za Brazil, kule Rio De Janeiro na Cape Town, South Africa kwa kutumia cable ili kuongeza mapato zaidi kupitia mlima huo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Mahawe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini tutaboresha miundombinu, tumekuwa tukichukua hatua mbalimbali za kuboresha miundombinu katika hifadhi zetu. Hili alilolipendekeza kuangalia uwezekano wa kuweka labda vitu kama cable car na vitu vinginevyo basi tutaliangalia kwa kadri bajeti itakavyoruhusu pale ambapo tunaweza kutekeleza ili liweze kuwavutia watalii wengi zaisi na kuweza kufanikisha hili jambo.