Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 10 Sitting 6 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 79 2018-02-06

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y. MHE. JAMES F. MBATIA) aliuliza:-
(a) Je, kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita Mlima Kilimanjaro umeliingizia Taifa mapato ya fedha kiasi gani kwa njia ya utalii?
(b) Je, ni asilimia ngapi ya mapato hayo yametumika kuweka miundombinu endelevu ya kuuhifadhi Mlima huo?
(c) Je, ni asilimia ngapi ya mapato hayo yametumika katika dhana nzima ya ujirani mwema katika kutoa huduma zinazokuza utu wa wananchi wanaozungukwa na Mlima huo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa James Francis Mbatia, Mbunge wa Vunjo, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Hifadhi Taifa Tanzania (TANAPA) ni Shirika la Umma ambalo limeanzishwa kwa Sheria Na. 482 ya mwaka 1959 na kufanyiwa marejeo na kuwa Sheria Na. 282 ya mwaka 2002. Shirika linatekeleza majukumu yake ya uhifadhi na kuendeleza utalii katika Hifadhi za Taifa 16.
Kati ya Hifadhi hizo ni hifadhi tano tu ndizo zinazokusanya mapato ya ziada yanayotumika kuendesha Hifadhi za Taifa nyingine 11. Hifadhi hizo ni Serengeti, Mlima Kilimanjaro, Tarangire, Ziwa Manyara na Arusha. Mapato yaliyotokana na Mlima Kilimanjaro na fedha zilizotumika kuweka maendeleo endelevu ya kuhifadhi mlima na kiasi kilichotumika katika dhana ya ujirani mwema kwa wananchi wanaozunguka mlima huo ni kama ifuatavyo:-
(a) Mapato ya Hifadhi ya Kilimanjaro katika kipindi cha miaka kumi, yaani kuanzia mwaka 2007/2008 hadi mwaka 2016/2017 ilikuwa ni shilingi bilioni 471.5.
(b) Fedha zilizotumika kutekeleza majukumu ya uhifadhi ikiwa ni pamoja na kuweka miundombinu ya kuendeleza mlima ni shillingi bilioni 67.5 ambazo kati ya hizo shilingi bilioni 20.89 zilitumika kwa maendeleo na shilingi bilioni
46.6 zilitumika katika uendeshaji wa hifadhi.
(c) Fedha zilizotumika katika kuendeleza miradi ya kijamii katika vijiji vilivyo jirani na Hifadhi ya Kilimanjaro ni shilingi bilioni 2.28.