Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Jimbo la Ulanga imezungukwa na Hifadhi ya Selous Game Reserve hivyo kufanya wananchi wa Kata za Mbuga, Ilonga, Kataketa na Lukunde kukosa maeneo ya kilimo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo maeneo ya kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa nafasi ya pekee napenda nikipongeze Chama changu cha Mapinduzi kwa kutimiza miaka 41 ya utawala bila kung’oka, na kwa utendaji huu tuna miaka 41 mbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri atakuwa shahidi tangu hili pori lianzishwe ni miaka mingi sasa na watu wameongezeka kwa kiasi kikubwa, sheria hizi zilizoanzisha mapori ndiyo sheria hizi hizi zilizoanzisha vijiji, inapotokea maeneo wanayoishi wananchi yakagundulika madini wananchi wanatolewa, lakini wananchi wanapohitaji kulima maeneo ya mapori wanaambiwa sheria zizingatiwe. Kwa nini sheria ziko bias upande mmoja kwa kuwaonea wananchi ambao ni wanyonge?
(b) Mheshimiwa Waziri tulikuwepo nae Ulanga wiki mbili zilizopita ameona jiografia ya Ulanga ilivyo ngumu maeno yote ya matambalale ambayo wananchi wanaweza wakalima ni Mapori Tengefu, ni Hifadhi na Bonde la mto Kilombero, naomba busara zitumike ili wananchi wapate maeneo ya kilimo kwa sababu wameongezeka kwa kiasi kikubwa.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa wakati tunapata Uhuru idadi ya wananchi wa Tanzania ilikuwa haizidi milioni tisa na ardhi ilikuwa hivi, lakini miaka karibu 56 ya Uhuru wananchi wa Tanzania wameongezeka kwa kiwango kikubwa sana, sasa tuko karibu milioni 52 lakini ardhi haijaongezeka. Kwa hiyo naomba nimuambie Mheshimiwa Mbunge kwamba kutokana na ongezeko la watu ndiyo maana kumekuwa na presha kubwa sana katika maeneo yaliyohifadhiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo naomba nimhakikishie kwamba sheria zilizotungwa sio kwamba ziko bias, sheria ziko vizuri kabisa, sheria zinaainisha maeneo yaliyohifadhiwa, maeneo ambayo yanafaa kwa makazi, maeneo yanayofaa kwa ufugaji, maeneo yanayofaa kwa kilimo kwa hiyo hili lazima tulisimamie ipasavyo. Siyo kwamba sheria zinapendelea labda kitu fulani na Serikali yetu itaendelea kuhakikisha kwamba wananchi wanapatiwa maeneo ya kulima yale yanayostahili na yale yaliyohifadhiwa yaendelee kuhifadhiwa kwa mijibu wa sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali lake la pili ni kweli kwamba tutatumia busara kubwa sana katika kuhakikisha kwamba wananchi wa Jimbo hili la Ulanga wanapata eneo la kulima, kufuatia hatua hiyo na ziara ambayo tumeifanya hivi karibuni kama alivyosema yeye mwenyewe Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii ameunda Kamati ya Wajumbe 22 kwa sababu ya ukubwa wa Bonde lenyewe la Kilombero lilivyo ili kuweza kubainisha, kuweza kupitia maeneo yote na waone ni maeneo gani yahifadhiwe, maeneo gani yatafaa kwa kilimo ili kusudi wananchi wapate kuelekezwa ipasavyo. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Jimbo la Ulanga imezungukwa na Hifadhi ya Selous Game Reserve hivyo kufanya wananchi wa Kata za Mbuga, Ilonga, Kataketa na Lukunde kukosa maeneo ya kilimo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo maeneo ya kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBER M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vya Mpigamiti pamoja na Kikulyungu ni vijiji ambavyo vimepakana na hifadhi ya Selous katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, lakini kuna mgogoro mkubwa sana wa ardhi kati ya Kikulyungu pamoja na Selous.
Je, ni lini Mheshimiwa Waziri utaweza kutatua mgogoro huu ambao umedumu zaidi ya miaka 10 na watu tayari washapoteza maisha?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika eneo hili kuna migogoro mingi na kuna eneo kubwa ambalo kwa kweli kuna matatizo. Naomba nikuhakikishie hata jana nilikuwa karibu na pori la Selous katika maeneo ya Mbwande nikishughulikia matatizo ambayo yanafanana na namna hii. Kwa hiyo, katika eneo lako hili la Mpigamiti pamoja na Kikulyungu ambako kuna matatizo naomba niseme kwamba ninalichukua tutaendelea kulifanyia kazi na tutashirikiana na wewe ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa hili tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu kusudi wananchi wa eneo lako wapate kufaidika na wapate kufurahi. (Makofi)

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GOODLUCK A. MLINGA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Jimbo la Ulanga imezungukwa na Hifadhi ya Selous Game Reserve hivyo kufanya wananchi wa Kata za Mbuga, Ilonga, Kataketa na Lukunde kukosa maeneo ya kilimo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia wananchi wa maeneo hayo maeneo ya kilimo?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, takribani zaidi ya vijiji 12 vinavyozunguka Pori la Akiba la Mkungunero hawafanyi kazi ya kilimo kwa sababu ya mgogoro mkubwa ambao umedumu zaidi ya miaka 10, kati ya wafanyakazi wa pori la Akiba la Mkungunero na wakulima wanaozunguka pori lile. Suala hili limeshafika Serikalini, lakini hakuna hatua zinazochuliwa. Wabunge wa Majimbo Mheshimiwa Juma Nkamia na Mheshimiwa Dkt. Ashatu wanapata shida sana wakati wa kampeni na hata wakati wa kuwatembelea wananchi wao.
Je, ni lini sasa matatizo haya yatakwisha mpaka halisi wa pori la Mkungunero litabainishwa ili wakulima wale wafanye kazi yao kwa uhuru na kwa amani?(Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwa na tatizo la muda mrefu la vijiji hivi 12 katika pori la Akiba la Mkungunero ambapo wananchi walikuwa wanagombania mipaka, hili ni mojawapo ya eneo ambalo Kamati ya Kitaifa imeyapitia na wenyewe tumeipitia tumeona kweli kuna mgogoro ambao unatakiwa kutatuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie fursa hii kumuomba Mheshimiwa Felister Bura kwamba katika hili eneo Serikali iliagiza kwamba maeneo yote yenye migogoro yawekewe mipaka na muda wa mwisho ulikuwa ni tarehe 31 Desemba, 2017. Hivi sasa tunafanya tathmini kupitia maeneo yote sio tu katika eneo hili la Mkungunero, katika mapori yote ya akiba na mengine yote kuangalia baada ya kuweka mipaka na vigingi katika haya maeneo ni maeneo yapi ambayo yana migogoro, ni maeneo kiasi gani tunatakiwa tuyaachie ama tuendelee kuyahifadhi na wananchi watafutiwe maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya haya yote kukamilika basi Waheshimiwa Wabunge watajulishwa na hatimae tutajua kabisa kwamba wananchi sasa watatatuliwa haya matatizo na hili tatizo la Mkungunero na vijiji hivi 12 vyote vitakuwa vimepata ufumbuzi wa kudumu.